Treni ya kisasa ikiwa safarini 
            
Posted Alhamisi,Agosti29 2013 saa 12:50 PM
Kwa ufupi
Watafiti wa masuala ya kiuchumi wanasema 
bandari hii ni lango kuu la biashara ya kimataifa kwa nchi za Afrika 
Mashariki na Kati ambazo hazina bahari na kama ingekuwa na ufanisi kama 
ilivyo Bandari ya Mombasa, uchumi wa Tanzania ungeingiza takriban Dola 
za Marekani 1.8 bilioni kwa mwaka (Sh2.88 trilioni) sawa na asilimia 7 
ya Pato la Taifa (GDP) kwa sasa.
Bandari ya Dar es Salaam; rasilimali nyingine ambayo Tanzania imejaliwa katika mwambao wa Bahari ya Hindi.
Watafiti wa masuala ya kiuchumi wanasema bandari 
hii ni lango kuu la biashara ya kimataifa kwa nchi za Afrika Mashariki 
na Kati ambazo hazina bahari na kama ingekuwa na ufanisi kama ilivyo 
Bandari ya Mombasa, uchumi wa Tanzania ungeingiza takriban Dola za 
Marekani 1.8 bilioni kwa mwaka (Sh2.88 trilioni) sawa na asilimia 7 ya 
Pato la Taifa (GDP) kwa sasa.
Mbali na hayo linapokuja suala la usafirishaji wa 
shehena za mizigo kwenda au kutoka ughabuni; Zambia, Uganda, Rwanda, 
Burundi, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC) na Malawi wanatumia 
Bandari ya Dar es Salaam ili kufikia lengo hilo.
Zambia inatumia bandari hiyo kwa asilimia 46.6, Burundi (9.1), Rwanda (8.5), Malawi(4.1) na nyingine asilimia 9.8.
Takribani asilimia 90 ya biashara ya kimataifa ya Tanzania hupita katika Bandari ya Dar es Salaam.
Wakati bandari hiyo ikionekana kuwa muhimu kiasi 
hicho, hivi karibuni vyombo vya habari viliripoti kuwa nchi za Uganda na
 Rwanda zitasitisha kutoitumia bandari hiyo kuanzia mwezi Septemba.
Kwa mujibu wa Chama cha Wasafirashaji wa Mafuta 
nchini(Tatoa), nchi hizo zimekuwa zikiilalamikia bandari hiyo lakini 
hakuna hatua zozote zimechukuliwa na serikali kutatua matatizo hayo.
Takriban asilimia 90 ya biashara ya kimataifa ya Tanzania hupita katika Bandari ya Dar es Salaam.
Wakati bandari hiyo ikionekana kuwa muhimu kiasi 
hicho, hivi karibuni vyombo vya habari viliripoti kuwa nchi za Uganda na
 Rwanda zitasitisha kutoitumia bandari hiyo kuanzia mwezi Septemba.
Kwa mujibu wa Chama cha Wasafirishaji wa Mafuta 
nchini(Tatoa), nchi hizo zimekuwa zikiilalamikia bandari hiyo lakini 
hakuna hatua zozote zimechukuliwa na Serikali kutatua matatizo hayo.
Moja ya malalamiko yanayotajwa ni wafanyabiashara 
kucheleweshewa mizigo yao katika bandari hiyo na kuwapo kwa vizuizi 
vingi kwenye barabara za Tanzania.
Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe anasema 
nchi hizo haziwezi kujitoa katika Bandari ya Dar es Salaam kwani umbali 
kutoka Kigali hadi Dar es Salaam ni zaidi ya kilometa 1,460) wakati 
kutoka Kigali hadi Mombasa ni kilometa 1,704 ilipo bandari nyingine 
ambayo inatarajiwa kutumiwa na Rwanda.
Waziri anabainisha kwamba inachukua saa 18 kutoka Dar es Salaam hadi Kigali wakati Kigali mpaka Mombasa ni saa 25.
Dk Mwakyembe anakiri kwamba kuna vizuizi 56 katika barabara inayotoka Dar es Salaam hadi Rusumo mpakani mwa Rwanda na Tanzania.
Kutokana na vizuizi hivyo Serikali ina mpango wa 
kuvipunguza na kubaki vitatu, lakini pia anasema atawasiliana na waziri 
mwenzake wa Rwanda mwenye dhamana ya Uchukuzi kwa ajili ya kuzungumzia 
suala hilo.
Rwanda, Uganda kujenga reli
Wakati bandari hiyo ikisifika kwa kutokuwa na 
tija, Juni Rais Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda na 
Uhuru Kenyatta wa Kenya walikutana mjini Entebe Uganda na kwa pamoja 
walipitisha uamuzi wa kujenga reli itakayounganisha Miji ya Mombasa, 
Kampala na Kigali.
Ujenzi wa reli hiyo una thamani ya Dola 13 bilioni
 za Marekani na unatarajiwa kukamilika mwaka 2018 na mpango huo unatajwa
 kuwa muhimu katika kusafirisha mizigo kutoka Bandari ya Mombasa hadi 
Kigali.
Ujenzi huo bila shaka utaleta changamoto katika 
Bandari ya Dar es Salaam ambayo inaonekana kuwa na matatizo chungu 
nzima, ambayo yamesababisha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) 
kukataa kupitisha ripoti ya Hesabu ya Mamlaka ya Bandari (PTA) kutokana 
na ubadhilifu wa Sh57.6 bilioni.
Kwa upande wa Tanzania, Dk Mwakyembe anasema 
mikakati inaendelea ya kuiboresha reli ya kati na itakapokamilika 
itasaidia kusafirisha mizigo kupeleka maeneo mbalimbali zikiwamo nchi 
jirani.
Waziri Mwakyembe anafafanua kuwa watahakikisha 
hadi kufika mwaka 2015 Bandari ya Dar es Salaam, inakuwa na uwezo wa 
kuingiza tani milioni 12 hadi tani milioni 18 kwa mwaka.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti kuhusu 
Kuondoa Umaskini (Repoa), Profesa Samuel Wangwe anasema ujenzi wa reli 
ya nchi hizo tatu hautaathiri sana uchumi kwani kuna umbali mrefu kutoka
 Mombasa hadi Kigali.
Profesa Wangwe anasema kuna umuhimu wa kujenga 
reli inayotoka Kigoma kwenda nchi za Kongo (DRC) na Burundi ili 
kurahisisha usafirishaji wa mizigo.
Profesa huyo anasema Bandari ya Dar es Salaam 
inaweza kuwa kitovu cha biashara katika nchi za ukanda wa Afrika 
Mashariki na Kati, lakini ili ifikia katika kiwango hicho hakuna budi 
kufanya kazi kisasa.
“Mizigo ishughulikiwe haraka na watumie taknolojia za kisasa,” anasema Profesa Wangwe.
Vizuizi barabarani
Profesa Wangwe anasema ili kuongeza ufanisi zaidi,
 mambo matatu yanapaswa kutazamwa ambayo ni kuondoa rushwa, kutumia 
teknolojia ya kisasa katika bandari hiyo na kupunguza vizuizi vya 
ukaguzi barabarani.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa 
Joseph Mbele anasema Tanzania inapaswa kufanya utafiti ili kupunguza 
gharama za uendeshaji na kuleta ushindani.
Utafiti uliofanywa na mtandao unaojihusisha na 
ukaguzi wa hesabu KMPG na Benki ya Dunia(WB) unaonyesha kwamba Mei na 
Juni 2012, meli zilizokuwa zimebeba makontena zilikuwa zinapanga foleni 
kwa wastani wa siku 10 ili kusubiri gati katika Bandari ya Dar es 
Salaam, wakati muda wa kusubiri ulikuwa chini ya siku moja katika 
Bandari ya Mombasa.
Pia utafiti huo unasema siyo tu kwamba Bandari ya 
Dar es Salaam haina ufanisi, lakini pia ina gharama kubwa kwa asilimia 
74 kuliko Mombasa na kusababisha kampuni nyingi za meli, kulazimika 
kulipa ada zaidi kwa mawakala kuliko Bandari ya Mombasa.
Ripoti hiyo inaweka wazi kuwa kama hali ya sasa 
haitapatiwa ufumbuzi, Bandari ya Dar es Salaam inaweza kupoteza nafasi 
yake katika biashara ya ukanda wa Afrika Mashariki na kati.
source : Mwananchi
source : Mwananchi