TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO TASAO
Wednesday, 6 April 2011
Mkutano Mkuu wa TASAO na Uchaguzi wa Viongozi Wapya
Friday, 31 December 2010
TAARIFA YA MSIBA
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.
Thursday, 22 July 2010
Thursday, 15 July 2010
Sunday, 27 June 2010
HAVE YOU EVER VISITED RUAHA NATIONAL PARK? HERE ARE SOME CLUES


Tuesday, 22 June 2010
Friday, 11 June 2010
Bajeti ya Kilimo Kwanza
11th June 2010
- Kodi zake kibao zafutwa
- Za bia, sigara, magari juu
- Petroli, dizeli zapona
Serikali imetangaza bajeti mpya ya mwaka wa fedha wa 2010/11 ambayo imejielekeza kusaidia zaidi wakulima na wafugaji kwa kuwaondolea kodi mbalimbali, lakini imeendelea na jadi yake ya kuongeza kodi kwenye bia, vinywaji baridi, mvinyo, pombe kali, sigara na usajili wa magari.
Akiwasilisha bajeti hiyo bungeji jana jioni, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mukulo, alisema ongezeko la kodi hizo ni la asilimia nane kiwango ambacho hakizidi mfumuko wa bei.
Katika bajeti hiyo, mafuta ya petroli na bidhaa zake zote kodi zake hazijaguwa. Hata hivyo kuna punguzo mafuta ya kuendesha mitambo kutoka Sh. 97 hadi 80 kwa lita.
Ongezeko la viwango hivyo na vile vya zamani kwenye mabano ni vinywaji baridi Sh. 63 kwa lita (Sh. 58) na bia inayotengenezwa na nafaka ya hapa nchini na ambayo haijaoteshwa Sh. 226 kwa lita (Sh. 209) wakati bia nyingine zote zimepanda kutoka Sh. 354 kufikia Sh 382 kwa lita.
Alisema mvinyo unaotengenezwa kwa zabibu inayozalishwa nje ya nchi kwa kiwango kinachozidi asilimia 25 itakuwa Sh. 1,223 kwa lita (Sh 1,132) na vinywaji vikali itakuwa Sh. 1,812 kwa lita (Sh. 1,678).
Kwa upande wa sigara, Mkulo alisema zile zisizokuwa na kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75 itakuwa Sh. 6,209 kwa sigara 1,000 (Sh. 5,749).
Kwa sigara zenye kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa hapa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, itakuwa Sh 14,649 (13,564).
Alisema sigara nyingine zenye sifa tofauti na hizo, itakuwa Sh. 26,604 kwa sigara 1,000 (Sh. 24,633).
Wakati huo tumbaku ambayo ipo tayari kwa utengezaji wa sigara itakuwa Sh. 13,436 kwa kilo (12,441 na ushuru wa cigar unabaki kuwa asilimia 30.
“Hatua hizi katika ushuru wa bidhaa kwa pamoja zinatarajiwa kupunguza mapato ya serikali kwa kiasi cha Sh. bilioni 20.042,” alisema.
Mkulo alisema serikali imesamehe kodi ya majengo kwa nyumba wanamoishi wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60, ambao hali zao kiuchumi haziwawezeshi kulipa kodi hiyo.
“Hata hivyo msamaha huo utatolewa kwa wale watakaothibitishwa na uongozi katika serikali za mitaa kuwa kweli hawana uwezo wa kulipa kodi husika,” alisema.
Pia alisema kiwango cha kutoza ushuru wa mazao shambani kitakuwa kati ya asilimia 3 na 5 ya bei ya kuuza mazao mashambani, ili kuzipa fursa halmashauri na serikali za mitaa kutoza ushuru huo kulingana na uwezo na rasilimali zilizopo.
Ada ya usajili wa magari na pikipiki
Alisema usajili wa magari unatapanda kutoka Sh. 120,000 hadi Sh. 150,000 wakati pikipiki itakuwa Sh. 45,000 ikilinganisha na Sh 35,000 za awali.
Mkulo alisema hatua hizo zitaongeza mapato ya serikali kwa Sh. bilioni 3.19
Ada ya mwaka ya leseni
Kwa upande wa ada ya mwaka ya leseni za magari itakuwa Sh. 50,000 badala ya Sh. 30,000 kwa gari lenye ujazo wa injini 0-500cc.
Gari lenye ujazo wa injini 501 hadi 1,500cc, itapanda kutoka Sh. 50,000 hadi kufikia Sh. 100,000 wakati lenye ujazo wa kati ya 1501-2,500 itakuwa Sh 150,000 badala ya Sh 100,000.
Kwa upande wa gari lenye ujazo wa injini zaidi ya 2,501 ada itakuwa Sh 200,000 badala ya Sh. 150,000 ya sasa.
“Hatua hizi katika kuongeza viwango vya ada ya mwaka ya leseni za magari kwa pamoja zinatarajiwa kuongeza mapato ya serikali kwa kiasi cha Sh. bilioni 16.981,” alisema.
Usafirishaji korosho
Mkulo alisema kutakuwa na ongezeko la ushuru wa kusafirisha korosho ghafi kutoka asilimia 10 ya sasa hadi 15 (ama Dola 160 za Marekani) kwa tani moja.
Alisema lengo la ongezeko hilo ni kulinda viwanda, kuongeza ubora na thamani ya korosho na kukuza ajira kwa wananchi.
Kwa mujibu wa Mkulo hatua hiyo inatarajiwa kuongeza mapato ya serikali kwa Sh bilioni 2.613.
Michezo ya kuhabatisha
Mkulo alisema kiwango cha kodi inayotozwa kwenye mashine za michezo ya kubahatisha itaongezeka kutoka Sh. 16,000 hadi 32,000 wakati kodi ya kiwango cha asilimia 13 ya mapato itatozwa katika mashine ya tombola, hivyo kuongeza mapato ya serikali kwa Sh. bilioni 0.5.
Misamaha wa kodi
Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka shambani hadi kwenye viwanda vya usindikaji kwa wakulima wenye kilimo cha mkataba wa miwa, mkongwe na chai imesamehewa.
Kodi nyingine iliyosamehewa ni VAT katika mashine na vifaa vya vya kukusanya, kusafirisha na kusindika maziwa ili kuhamasisha uwekezaji katika sekta ndogo ya maziwa na kuboresha kipato kwa wananchi.
Mashine na vifaa vitakavyohusika katika msamaha huo ni vifaa maalum vya kubebea maziwa, pampu maalum za kusukumia maziwa na bomba maalum la kupitishia maziwa kwenye viwanda vya usindikaji.
Vifaa vingine vilivyopata msamaha huo ni kompresa maalum zinazotumika kwenye vifaa vya kupoza maziwa, matanki ya kuhifadhia maziwa gari maalum lenye kifaa cha kupoza na kusafirisha maziwa.
Vingine ni mtambo maalum wa kuchemsha maziwa ili kutoa siagi, vifaa maalum vya kupoza na kutengeneza ubaridi na kifaa maalum cha kukandamiza na kukamua maji ili kuzalisha jibini.
Mkulo alisema msamaha mwingine umetolewa kwenye mashudu kwa ajili ya chakula cha mifugo.
Hatua hiyo inalenga kuhamasisha ufugaji bora na kuwawezesha wakulima wa mbegu za mafuta kupata bei yenye tija kwa mauzo ya bidhaa hiyo.
Pia, serikali imetoa unafuu maalum wa VAT kwa vifaa vinavyouzwa kwa watalaam wa mifugo waliosajiliwa.
Vitu vingine vilivyosamehewa VAT ni zana za kilimo kama kivuna nafaka, pick up balers, mashinde ya kufunga majani ya ng’ombe (hay making machinery) na mowers vinavyotumika mahsusi katika uzalishaji wa kilimo na mifugo.
Sekta ya kilimo cha maua nayo imenufaika na msamaha wa VAT kwa ufarishaji wa maua kwa ndege kwenda nje ya nchi, kwa mabanda (green house) yanayotumika katika kilimo cha maua.
Bajeti hiyo inaonyesha pia kutoa unafuu maalum wa VAT katika uuzaji wa bidhaa na huduma zinazotolewa kwa wakulima waliosajiliwa ama mashamba ya vyama vya ushirika na ujenzi wa miundombinu ya mashamba.
Miundombinu hiyo ni pamoja na mitaro ya umwagiliaji, barabara za mashambani, ujenzi wa maghala au huduma nyingine zinazofanana na hizo.
Pia msamaha wa VAT umetolewa kwa huduma za kuzalisha mifugo kwa njia ya kupandisha mifugo na kutumia mashine maalum za kuzalishia ama kutotolea vifaranga.
Mkulo alisema ili kuhamasisha uwekezaji na uzalishaji katika sekta ya viwanda nchini, unafuu maalum wa VAT umetolewa kwa waendelezaji wa maeneo yenye uwekezaji kwenye bidhaa za kuuza nje yaani EPZ na SEZ.
Mkulo alisema kutakuwa na tozo la VAT kwa asilimia sifuri katika usindikaji na uzalishaji wa mafuta ya kula kwa wazalishaji wanaotumia mbegu za mafuta zinazozalishwa hapa nchini.
Alisema VAT imesamehewa katika vifungashio vya juisi za matunda na bidhaa za maziwa.
“Hatua hii inalenga katika kupunguza gharama za uzalishaji na kuboresha thamani ya bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda vya juisi na maziwa hapa nchini,” alisema.
Mkulo alisema serikali imerejesha utaratibu wa kutambua baadhi ya vifaa kama bidhaa za mtaji kwa wawekezaji ili kuvipa nafuu ya kodi.
Hata hivyo, alisema serikali itaunda kamati maalum ya kushughulikia suala hilo, ili kudhibiti matumizi mabaya ya utaratibu huo yanayoweza kuvujisha mapato.
Alisema hatua hizo zinazohusu VAT zitasababisha kupungua kwa mapato ya serikali kwa kiasi cha Sh. bilioni 2.39.
Kuhusu sheria ya kodi ya mapato sura 332, Mkulo alitoa kauli ya kurekebisha kifungu cha 11 cha sheria hiyo ili kuweka wigo wa ukomo wa maeneo ya uchimbaji wa madini.
Alisema nia ni kudhibiti gharama zinazotakiwa kutolewa katika kukokotoa faida, itakayotozwa kodi ya mapato kwa eneo husika.
Pia kutokana na kuwepo biashara nyingi zinazofanywa na watu wasiokuwa na namba za utambulisho wa mlipa kodi (Tin), alipendekeza kodi ya zuio inayozuiwa na serikali kwa wauzaji wa bidhaa na watoa huduma wasiokuwa na Tin, izuiwe.
Mkulo alitangaza punguzo la ushuru wa bidhaa kwenye mafuta mazito ya kuendesha mitambo kutoka Sh. 97 hadi 80 ili kupunguza gharama za uzalishaji wa bidhaa hapa nchini.
Alisema hatua hiyo imezingatia ridhaa ya serikali kukuza viwanda, ajira na mapato ya ndani.
Pia alisema punguzo hilo limezingatia makubaliano ya serikali na wenye viwanda kupunguza ushuru huo na hatimaye kuufuta katika kipindi cha miaka mitatu.
Waziri huyo aliomba Bunge liidhinishe Sh. milioni 11,609,557 kati ya hizo matumizi ya kawaida ni Sh. milioni 7,790,506 na za maendeleo ni Sh. milioni 3,819,051.
Monday, 7 April 2008
MKUTANO MKUU KATIKA PICHA - 29.03.2008
BAADA YA MKUTANO MKUU
Baadhi ya maamuzi ya msingi ni:
1. Tarehe ya mahafali ya kuwaaga wanaomaliza muda wao wa masomo ilikubaliwa iwe ni: 9.may.2008
2. Uchaguzi wa viongozi wapya. Wafuatao walichaguliwa kuwa viongozi wa TASAO kwa mwaka 2008/2009
Nafasi Majina
Rais - John Chaluklu
Makamu - Rais Rose Matete
Katibu - Jane Bakahwemama
Mweka hazina - C. Lwiza
Accademic+ Recreation - Ernest Mjigo na Br. Nikuli
Afya na Ustawi - Said Bakari na Stela Bitanyi
Wajumbe Kamati ya fedha - Beatrice Chinguwile, Jelly Jerry
Wajumbe TASAO - Hezron Nonga na Julitha John
Uongozi uliotangulia unawshukuru wajumbe wote kwa ushirikiano wenu na unawaomba muendeleze ushirikiano zaidi kwa viongozi wapya!
Thursday, 20 March 2008
MKUTANO MKUU WA WANACHAMA WOTE

Tuesday, 12 February 2008
Baraza Jipya la Mawaziri - Tanzania - 12.Feb. 2008
Thursday, 7 February 2008
BREAKING NEWS!!!!!
Mh.. EDWARD LOWASA (PM)HABARI TOKA DODOMA SASA HIVI ZINASEMA KUWA SPIKA WA BUNGE MH. SAMWEL SITTA AMETANGAZA KWAMBA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA AMEAMUA KUJIUZULU UWAZIRI MKUU.
MH. SPIKA BAADA YA KUTANGAZA HILO AMESEMA MJADALA WA RIPOTI YA RICHMOND, NA SIO MJADALA WA LOWASSA, NDIO UENDELEE. NA NDICHO KINACHOFANYIKA HIVI SASA HUKO BUNGENI.
HABARI ZAIDI ZINASEMA KWAMBA MH. LOWASSA AMESEMA KWAMBA INGAWA HAJAMTAARIFU JK UAMUZI WAKE HUO, AMEAMUA KUJIWEKA KANDO.
Wednesday, 6 February 2008
Mambo ya RICHMOND hayooooooo!!!


Jengo jipya la Bunge Dodoma
Haya sasa ile ripoti ya ubadhilifu wa mamilioni ya fedha za walalahoi sakata la Richmond hii hapa!
Kong'oli hapa http://watanzaniaoslo.blogspot.com/.
Monday, 3 December 2007
ADA YA KILA MUHULA
Mnakumbushwa kuhusu kuwakilisha ada za uanachama za kila muhula kwa mhazini wetu. Kama hutaweza fanya hivyo, waweza mpatia kiongozi yeyote na mchango wako utafika mahala unapohitajika kufika.
Ada ni 200NOK
Ahsante kwa ushirikiano wako!
Mhazini - TASAO
Friday, 9 November 2007
INVITATION
Dr. Kenneth D. Kaunda
Voksenåsen Oslo
Ullveien 4, 0791 Oslo
http://www.voksenaasen.no/
K.K. Is coming to Norway to attend an international conference:
“A Dialogue conference on the unpredictable past and future of genocide,”
which is to be held at Voksenåsen November 16 and 17. To mark this occasion, Voksenåsen in collaboration with Networkers South North is hosting a reception and meeting with Dr. Kenneth D. Kaunda.
One remembers Kenneth David Kaunda for his important role in the fight against colonial powers, apartheid in Southern Africa throughout several decades of the 20th century. Kenneth Kaunda is 83 years old and is still active both in political diplomacy and in the fight against HIV/AIDS.
It is crucial that guests RSVP by Sunday, November 9 to confirm their attendance to the of the following email address:
bagandatz@yahoo.co.uk.
Food and Drinks will be served for free!!!!
On Behalf of Networkers and Voksenåsen
Karl Einar Ellingsen and Øystein Tveter
Tuesday, 16 October 2007
'Sex Play' in kindergartens - Watanzania mpooh!!

Norwegians woke up Tuesday morning to news that a respected Oslo pre-school teacher, backed by child psychologists, thinks children should be allowed to openly express their own sexuality, not least through sex play and games in the local day care centers known as barnehager, or kindergartens.
The vast majority of Norwegians send their children from the age of one to the kindergartens, where they spend their days until they begin school at age six.
Pia Friis, leader of the popular Bjerkealleen Barnehage in Oslo and a well-known pre-school educator, told newspaper Dagbladet on Tuesday that children should be allowed to express their own sexuality at day care centers. She doesn't want to stifle what comes naturally.
Children, she said, should be able "to look at each other and examine each other's bodies. They can play doctor, play mother and father, dance naked and masturbate.
"But their sexuality must also be socialized, so they are not, for example, allowed to masturbate while sitting and eating. Nor can they be allowed to pressure other children into doing things they don't want to."Friis said there's a lot of uncertainty around how day care center employees should handle children's sexuality.
"The only thing that is absolutely certain is that children, sooner or later, will play sexual games and examine each other at the kindergarten," she told Dagbladet. "When the personnel are uncertain, that passes on to the children, and it can be negative."
The issue is the topic of an article in the latest edition of the magazine published by Norway's industry association for privately owned kindergartens, PBL-nytt, and Friis thinks it's important. So do child psychologist Thore Langfeldt and family therapist Jesper Juul. "Children must learn about sexuality, otherwise things can go very wrong," said Langfeldt. "Children can't object to something they don't know about, and children can more easily and readily report assaults if they already are aware of their own sexuality." Juul conceded that "many are disturbed by children's sexuality, but I think it's important to put it on the agenda. That, in fact, is what we're doing."
While Norwegians are known for being liberal and tolerant, the issue already has sparked heated debate on radio programs and in online opinion forums. And some politicians are outraged, not least those on the conservative side. "I thought at first that this was a joke," said Karin Ståhl Woldseth, a spokesman on family issues for the Progress Party.
"Sexual games don't belong in a kindergarten," she declared. "Children don't need more exposure to this in kindergartens. We think it will damage their health."
Source: Aftenposten English Web Desk
Wednesday, 5 September 2007
SHUKRANI KWA FARAJA ZENU
Mzee wa mawe,
James Apolkarpi
Mob#: +255 754 588706
Email: james2001tz@ yahoo.com
03.09.2007
Tuesday, 7 August 2007
Kwa wanaopenda kujiendeleza kielimu!
1. All Tanzanians who are interested are called to apply. AtNIMR there are opportunities for Scientists and other staff. See the list of 46 Universities below. I have to say that please let as many people you know as possible apply (even outside of NIMR) - as most people may not have this information. In each University, there are procedures for application -the web page in Norwegian (click English) - to see the info in English. Then go to prospective students, then choose Quota program then make two choices. Initially you will fill in preliminary appl. - then they will send you the appl. forms through email.
2. Academic requirements: Basic training with General Pass Average (GPA) of 3.5 (Upper Second) and above - those with 1st Class usually are selected as policy. In addition, indication of Work experience is important. (Not mandatory as there are many Masters’ students studying here just fresh from Schools in Tanzania.
3. Sponsorship: These programs are fully sponsored. Education in Norway is free- so no tuition fees! The government will give you stipend to support food, travel accommodation etc. There are three main sponsorship arrangements:
I. Quota- this is the largest-
II. NOMA (formerly NORAD) - this is mainly for Masters and students do their studies either in South Africa or Makerere – Uganda but get funds as if they are studying in Norway.
4. Deadline for Application is 1st of December. All application forms together with letters of support, original certificates and other information should reach the Universities by this date.
5. Best places for NIMR Scientists/ Support staff.
i. University of Bergen
ii.University of Oslo
iii.University of Trøndheim
iv.University of Trømso
For Administrators at NIMR- Masters of Public Administration in Bergen and Oslo are very good courses- there are students from Mzumbe, from Uganda, Ghana etc.
6. PhD Program requirements: A protocol addressing priority problems is needed. From experience- Universities in Norway don’t accept other Masters from other countries for PhD directly- you will need one year to be assessed for Masters and in the second year you can switch to PhD program. If you have Masters in Norway you will be accepted directly- PhD prog. is three years- If you have Masters from elsewhere PhD prg. is 4 years. In the PhD prog. while studying in Norway req. is publication of 3 or 4 articles in peer reviewed journals.
7. If you are interested- or you have relative or friend, someone you know, with good qualifications- please pass the info. If you are unable to get the forms- feel free to contact TASAO or any Tanzanian student studying in Norway.
We encourage as many Tanzanians as possible to apply!
Academic institutions in the Quota Scheme







