Kwa ufupi
Alisema kikao cha baraza la mawaziri 
kinatarajia kupokea ripoti kuhusu maombi hayo, ambapo tayari timu ya 
maofisa wa jumuiya hiyo ilikwenda Sudan Kusini kutazama kama ina sifa za
 kujiunga na jumuiya hiyo.
Arusha. Nchi za Sudani Kusini na Somalia, 
zimeomba kujiunga na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki(EAC) na tayari 
mchakato wa kupitia maombi hayo umeanza.
Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Dk Richard Sezibera 
alitoa taarifa hiyo jana katika kikao na waandishi wa habari, wakati 
akielezea kuanza kikao cha baraza la mawaziri wa jumuiya hiyo.
Alisema kikao cha baraza la mawaziri kinatarajia 
kupokea ripoti kuhusu maombi hayo, ambapo tayari timu ya maofisa wa 
jumuiya hiyo ilikwenda Sudan Kusini kutazama kama ina sifa za kujiunga 
na jumuiya hiyo.
Alisema kwa upande wa Somalia, baraza hilo 
linatarajia kuridhia uamuzi wa Sekretarieti ya jumuiya ya kutuma maofisa
 wake kwenda Somalia kutazama kama ipo tayari kujiunga .
Aidha alisema hadi nchi hizo kukubaliwa kuwa mwanachama kuna mchakato mrefu zitapitia.
source: Mwanachi
source: Mwanachi