05: Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za 
Mitaa, Agrey Mwanri akiwaonyesha wananchi ufa za ukuta wa choo wa soko 
la Makuyuni Wilayani Korogwe Mkoani Tanga, ambapo zaidi ya Sh500 
milioni  zimeshatumika katika ujenzi wa soko hilo na bado halijakamilika
 na baadhi ya kuta za majengo  ziko hatarini kuanguka. PICHA | SALIM 
MOHAMMED 
            
    Na Salim Mohammed, Mwananchi
Posted Ijumaa,Oktoba4 2013 saa 19:17 PM
Posted Ijumaa,Oktoba4 2013 saa 19:17 PM
Kwa ufupi
- Ujenzi wa soko la Makuyuni ambalo lilianza  mwaka 
2008 na kutarajiwa kukamilika 2009, limeshindwa kukabidhiwa kwa 
halmashauri kwa kile kinachodaiwa kufanyika kwa ubadhirifu wa pesa za 
Serikali.
Korogwe. Naibu  Waziri, Ofisi 
ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Agrey 
Mwanri amemwagiza  Katibu Tawala  pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya 
Korogwe kuunda timu ya uchunguzi wa  ujenzi wa Soko la Makuyuni  unao 
daiwa kugharimu zaidi ya Sh500 milioni  huku  ujenzi huo ukishindwa 
kukamilika.
Ujenzi wa soko la Makuyuni ambalo lilianza  mwaka 
2008 na kutarajiwa kukamilika 2009, limeshindwa kukabidhiwa kwa 
halmashauri kwa kile kinachodaiwa kufanyika kwa ubadhirifu wa pesa za 
Serikali.
Akizungumza mara baada ya kulikagua soko hilo, 
Mwanri alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Korogwe, Lucas 
Mweri kuhakikisha ndani ya siku 30 soko hilo  linafanya kazi ikiwa  ni 
pamoja na kukamilisha ujenzi wake.
"Ndugu wananchi hapa kuna tatizo na siamini kuwa 
Sh500 milioni zimeshindwa kujenga kasoko haka na kuomba katibu tawala 
kuunda timu ya uchunguzi juu ya hili soko ...mimi siamini,” alisema 
Mwanri.
Mwanri alisema hatokuwa tayari kuona pesa za 
Serikali na  nguvu za wananchi zikifujwa na wajanja na kusema kuwa mtu 
yeyote anayefanya ufisadi atachukuliwa hatua na kurejesha pesa 
alizochukua.
Alisema soko hilo ambalo hata kukamilika kwake ni 
utata limeanza kukatika kuta zake pamoja na vyoo kubomoka na hivyo 
kuitaka kamati ya ujenzi kuwaeleza wananchi mamilioni ya pesa 
zilivyotumika.
Akisoma taarifa ya ujenzi huo, Mhandisi  wa soko 
hilo, Lucas Mweri, alisema ili kuweza kukamilika kwa ujenzi huo 
zinahitajika Sh28 milioni zaidi zikiwa ni pamoja na kuweka vizimba vya 
biashara.
Alisema soko hilo limeshindwa kukamilika baada ya 
kuishiwa pesa na hivyo kuitaka halmashauri kuidhinisha kiwango hicho ili
 kuweza kukamilisha ujenzi huo na kuanza wananchi kulitumia.
Alisema soko hilo ambalo litatumika kuuzia 
stakabadhi ghalani pamoja na wananchi kuuza na kununua bidhaa, litakuwa 
ni mkombozi  wa wakulima wa mahindi na mbogamboga wakiwamo wa makabichi 
na nyanya.
SOURCE: MWANACHI
SOURCE: MWANACHI