Na Frederick Katulanda, Mwananchi
Posted Septemba7 2013 saa 11:41 AM
Posted Septemba7 2013 saa 11:41 AM
Kwa ufupi
Mwanza. Mamlaka ya Usafirishaji ya Udhibiti
Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra),imeagiza wasafirishaji
wanaotumia vyombo vya majini kanda ya ziwa kupitia Bandari zote Ziwa
Victoria kusafirisha abiria mwenye kitambulisho.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,Meneja wa
Sumatra Kanda ya Ziwa, Mhandisi Japhet Ole Loisuimaye alisema, utaratibu
huo umelenga kuhakikisha kuna kuwa taarifa za kina kwa kila abiria
anayesafiri na meli ama boti ndani ya Ziwa Victoria.
Alisema utaratibu huo utaanza kutumika Septemba 9,
mwaka huu na kubainisha kwamba kila abiria atapaswa kuwa na moja kati
ya kitambulisho kifuatacho, Kitambulisho cha Uraia, cha Ukaazi, Paspoti,
cha Kupigia Kura, Kazi, Leseni ya Udereva ama kwa wale wasiokuwa na
hivyo vyote basi wawe na barua toka Serikali za Mitaa yenye picha.
“Agizo hili limetolewa na Serikali kwa lengo la
kuhakikisha kunakuwa na kumbukumbu sahihi za abiria (passenger manifest)
wote wanaosafiri na meli ama boti kwa umbali usiozidi maili za majini
(noutcal miles) 20 kati ya bandari, hivyo agizo hili halitawahusu abiria
wanaosafiri na vivuko,” alifafanua. Alisema agizo hilo linapaswa
kufuatwa na wasafirishaji wote kwa vile ni utekelezaji wa Kanuni za
Kuhakiki na kusajili abiria kama zilivyoainishwa.
source: Mwananchi
source: Mwananchi