Sunday 11 March 2007

ADA YA UANACHAMA




Napenda kuchukua nafasi hii kuwakaribisha rasmi ,kuanza kuwakilisha fees za tasao ,kama tulivyokubaliana katika kikao cha tarehe 24/ 02 / 07 ,na zilikuwa kama ifuatavyo;


(i) Ada ya kuingilia uanachamaHii ni ada itakayokupa uhalali wa kuwa mwanachama wa TASAOKikao kilipitisha NOK 100/=(ii) Ada ya kila semisterKikao kiliona kuwa ili kuepusha michango ya mara kwa mara ni vema kuwa na mchango wa kila semester. Kwa pamoja walikubali kuchanga NOK 200 kwa kila semister.

Hivyo basi kila mwanachama ,anaombwa kuwasilisha kiasi cha 300NOK
Ingekuwa ni vyema tuharakishe michango hii ,kama mnavyofahamu Graduation ni mwisho wa mwezi ujao ,Tungependa kufahamu mapema ,kiasi che fedha ili tujue kama kuna haja ya kuchangia Graduation au la.

Naomba ada hizo ziwakilishwe ,anwani hii Block 10 ,H0106 napatikana kuanzia saa moja jioni na kuendelea jumatatu mpaka jumapili.

Au waweza wasiliana na kiongozi yeyote aliye karibu nawe kwa kurahisiha zoezi hili hakikisha unapata taarifa za mawasilisho ya mchango wako kwa mhazini.

Asante sana Kwa ushirikiano wenu ,

Beatrice Chinguwile,
Mweka Hazina .
TASAO - (PAMOJA DAIMA)