Wednesday, 23 July 2008

Kuokota chupa za maji: 'Wendawazimu' au ujasiriamali?

AKIWA na lundo la chupa tupu za maji ya kunywa zilizokwishatumika, za kampuni tofauti, kijana Mohamed (si jina lake halisi), anapita mtaa hadi mwingine akiokota chupa tupu hizo na kuziweka katika kiroba.

Na akifanya hivyo, hasemi na mtu yeyote, macho yake wakati wote yanaangaza kuona ni wapi atapata anachokitafuta na kwenda kuziuza. Ni kazi ngumu, lakini anayoifanya kwa jitihada kubwa ingawa hali yake haibainishi hasa ni kipi anachopata katika biashara hiyo.

Mohamed ni mmoja wa makumi ya wengine wakiwamo kinamama, ambao kila siku wapo mitaaani wakikusanya chupa tupu za maji kwa ajili ya kwenda kuziuza kwa wafanyabiashara wa jumla, ambao nao wanaziuza katika viwanda zinakoyeyushwa na kutengenezwa bidhaa nyingine za plastiki.

Biashara hiyo iliyoshika kasi hivi karibuni, hususan jijini Dar es Salaam, wakati mwingine huleta maswali zaidi kuliko majibu iwapo kweli wanachopata kinalingana na mihangaiko yao hiyo, na kitaweza kubadili hali za maisha yao katika namna ya kupunguza umaskini kulingana na lengo la kwanza la milenia mwaka 2015.

Mwanasaikolojia mmoja katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambaye hapendi jina lake kutajwa gazetini, anasema kuwa kimsingi watu hao wanatafuta riziki lakini ana wasiwasi na aina hiyo ya ujasiriamali ambayo anasema kuwa pengine ingetambuliwa watendaji nao wangebadilika.

Anasema kuwa katika nadharia ya utafutaji ikiwa ni pamoja na kazi ambayo mtu anaifanya huwa ni lazima ifanye mrejesho ambao ni pato kwa mhusika, ambalo litaweza kubadili maisha yake hivyo ana wasiwasi kuwa kuna watu wananufaika kupitia migongo ya waokotaji hao.

“Kuna wakati kazi anayoifanya mtu inaweza kumuathiri na kwamba kuna watu wanaoifanya kazi hiyo wanaoelekea kuathirika pengine kutokana na 'nature' (asili) ya kazi yenyewe," anasema na kuongeza kuwa kazi hiyo ni kama nyingine lakini inatakiwa kuleta mabadiliko kwa watendaji.

Anasema kuwa mtu anaifanya kwa miaka miwili mitatu hali yake haibadiliki na mbaya zaidi anakuwa katika muonekana au mazingira ambayo yanaweza kumuingiza katika hatari ya kupata maradhi mengine basi hiyo haina tija kwake.

Mkazi mwingine wa jijini aliyejitambulisha kwa jina la Shaabani Ngigi, anabainisha kuwa kazi hiyo ina tatizo kutokana ukweli kuwa huhitaji lundo la chupa nyingi kuweza kupata kilo chache.
Anabainisha kuwa kilo moja haizidi sh 400. Anasema kuwa lundo kama hilo mtu si rahisi kulipata kwa siku moja ni lazima afanye kazi ya ziada - si kwa siku zisizopungua mbili hadi tatu akizunguka kote anakoweza kupita kutafuta chupa hizo.

"Fikiria kuna watu wanafamilia na anategemea biashara hiyo ya rejareja ambayo kwa siku kipato chake hakitoshelezi ikilinganishwa na nguvu unazotumia kuzitafuta," anasema na kuongeza kuwa wanaonufaika ni wale wanaoziuza jumla viwandani.

Ngigi anakiri kuwa wanamchango mkubwa katika kusaidia kuweka jiji katika hali ya usafi, lakini kampuni na wanunuzi wa jumla wanatakiwa kuwasaidia ama kwa kuboresha bei au vitu vingine vya namna hiyo, kutokana na ukweli kuwa siku za nyuma mtu ukiokota makopo au vitu vingine vya namna hiyo unaonekana 'mwendawazimu'.

Mfanyabiashara mwingine wa kuokota chupa hizo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mama Sarayu kutoka eneo la Jangwani, Dar es Salaam, anabainisha kuwa biashara hiyo ni kama nyingine, ina ugumu na unafuu wake, ila kikubwa ni kwamba mkate wa kila siku unapatikana.

Anasema kuwa yeye binafsi kila baada ya siku mbili au tatu za utafutaji hujikuta ameambulia sh 2000 zikiwa nyingi pato ambalo anakiri kuwa halifanani na ugumu wa kazi yenyewe. "Ndiyo hivyo tena watu tumejiajiri lakini ukweli ni kuwa ni kazi ngumu inayohitaji uvumilivu," anasema na kuongeza:

"Hata hivyo ninaishi kwa kutegemea biashara hiyo kutokana ukweli kwamba hakuna ajira na kuna wimbi kubwa la wasio na ajira za kueleweka".

Mjasiriamali huyo anabainisha kwamba suala la bei ni kitu ambacho kipo nje ya uwezo wao, kwa kuwa wanapanga wanunuzi kulingana na hali halisi ya soko na awali anakiri kuwa kazi hiyo ilifanywa zaidi na vijana ambao ama walikuwa wakionekana walevi wa vijiweni au watumiaji wa mihadarati.

"Zamani mateja ndio waliokuwa wakionekana kuzikusanya na kuziuza ili wapate pesa za kufanyia mambo yao, lakini sasa ni tofauti, wote tunatafuta ili kukidhi shida tulizonazo," anasema.

Mnunuzi wa jumla wa chupa hizo eneo la Temeke Chang'ombe, Ibrahim Nsaa, anasema uokotaji wa chupa tupu si wendawazimu, bali ni ajira kutokana na hali halisi ya maisha ilivyo hivi sasa.
Anasema kuwa yeye anayenunua kilo moja kwa sh 200 hadi 300, kwa wiki bila kutaja kiwango cha bei zake katika soko la jumla, anaeleza kuwa kuna watu ambao maisha yao yamebadilishwa na biashara hiyo.

Nsaa anabainisha kuwa kuna vijana na watu wengine ambao ni watumiaji wa mihadarati, ambao wamejitumbukiza katika biashara hiyo ili kupata pesa kwa ajili ya uraibu wao, ndio wanaoitia dosari biashara hiyo na kuifanya ionekane ya watu ambao wana matatizo ya akili.

"Zamani ilikuwa kuokota makopo ni wendawazimu lakini sasa ni tofauti - ni ajira," anasema na kwamba kimsingi ni mtu mwenyewe na malengo yake aliyojiwekea. Anasema kimsingi hakuna kazi mbaya, ila ni vile wewe mwenyewe utakavyojiweka na jinsi utakavyoifanya kulingana malengo yako.

Anasema kuwa kuna watu ni wajasiriamali wa jumla wa chupa hizo, lakini awali walianza kwa kuokota moja moja mitaani. Biashara hiyo imeonekana kuwa ngumu zaidi pale muhusika anapojikuta anatumika siku nzima huku na kujikuta anaambulia mfuko mmoja, ambao haufiki hata kila moja, hivyo kumfanya ajitume kwa wiki nzima kuhangaikia angalau apate kilo mbili.
Kuna wengine wanasema kwamba wanapata unafuu kidogo pale wanapoziponda, kwani huongeza angalau uzito kidogo lakini bila hivyo kilo tatu hujaza pick-up ambayo hupata pengine shilingi 1200 au chini ya hapo.

Kwa wastani biashara inayofanywa na wajasiriamali hao bila kujali anapata kilo ngapi kwa siku, ukweli unabaki kwamba ni ngumu na inahitaji kupewa thamani hasa kwa wanaonunua bidhaa hizo angalau kwa kuongeza kiwango cha malipo wanayonunulia, kwani kimsingi chupa hizo zina faida kwa wanaokwenda kuzalisha malighafi nyingine.
Source: Mtanzania Daima, 22.07.2008

Monday, 7 April 2008

MKUTANO MKUU KATIKA PICHA - 29.03.2008

Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa TASAO, 2008 katika picha:

Sehemu ya Wajumbe wa mkutano

Wasimamizi wa uchaguzi wakitoka mkutanoni

Uchaguzi ukiendelea

Wasimamizi wa uchaguzi wakisoma taratibu za uchaguzi

Baadhi ya wajumbe wa mkutano

Baadhi ya wajumbe wa mkutano

BAADA YA MKUTANO MKUU

Mkutano mkuu ulifanyika vizuri na kwa mahudhurio ambayo kwa kweli yaliridhisha sana. Kwa kifupi agenda zote zilijadiliwa vizuri na kukubaliwa na wajumbe.

Baadhi ya maamuzi ya msingi ni:
1. Tarehe ya mahafali ya kuwaaga wanaomaliza muda wao wa masomo ilikubaliwa iwe ni: 9.may.2008

2. Uchaguzi wa viongozi wapya. Wafuatao walichaguliwa kuwa viongozi wa TASAO kwa mwaka 2008/2009

Nafasi Majina
Rais - John Chaluklu
Makamu - Rais Rose Matete
Katibu - Jane Bakahwemama
Mweka hazina - C. Lwiza
Accademic+ Recreation - Ernest Mjigo na Br. Nikuli
Afya na Ustawi - Said Bakari na Stela Bitanyi
Wajumbe Kamati ya fedha - Beatrice Chinguwile, Jelly Jerry
Wajumbe TASAO - Hezron Nonga na Julitha John

Uongozi uliotangulia unawshukuru wajumbe wote kwa ushirikiano wenu na unawaomba muendeleze ushirikiano zaidi kwa viongozi wapya!

Thursday, 20 March 2008

MKUTANO MKUU WA WANACHAMA WOTE


Kutakuwa na mkutano mkuu wa wanachama wote na wanafunzi wapya.


Mahali: Norges Idrettshøgskole - Sognsvann (Sports School)


Tarehe: 29.03.2008


Muda: Saa 7:30 mchana - 11:00 jioni


Agenda:


1. Taarifa ya mwaka ya uongozi

2. Taarifa ya mhazini

3. Marekebisho ya katiba

4. Viongozi wapya

5. mengineyo


Wanafunzi wote wa kitanzania wanaosoma hapa Oslo - Norway mnakaribishwa!


Uongozi


Tuesday, 12 February 2008

Baraza Jipya la Mawaziri - Tanzania - 12.Feb. 2008

Rais JK ametangaza Baraza jipya la mawaziri, baada ya kuvunja baraza la mawaziri ya kufuatia Edward Lowasasa kujiuzulu baada ya kukumbwa na kashfa ya Richmond. Akizungumza katika ukumbi wa Tamisemi mjini Dodoma amesema baraza hilo limepunguzwa na kubakia na Mawazirii 26 badala ya 29 wa awali na Manaibu 21 badala ya 31.
Awali kabla ya kutangaza baraza hilo Rais Kikwete alisema kuna mawaziri walioomba kupumzika baada ya kutumikia serikali kwa muda mrefu na watabaki katika kushauri tu. ambao ni Mzee Kingunge Ngombare Mwiru, na Joseph Mungai.
1. (Menejimenti utumishi wa umma) - Hawa Ghasia.
2. (Ofisi ya Rais muungano) - Seif Mohamed Khatib.
3. (Mazingira) - Batilda Burian.
4. (Ofisi ya waziri mkuu utaratibu wa bunge) - Philipo Marmo.
5. (Tamisemi Tawala za mikoa na serikali za mitaa) - Stephen Wasira, naibu Serena Kombani. 6. 6. (Wizara ya mipango na Fedha) - Mustafa Mkulo, manaibu Jeremia Sumari na Omari Yusuph Mzee.
7. (Afya na ustawi wa jamii) - Prof. Mwakyusa, Naibu Asha Kigoda.
8. (Ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi) - John Chiligati.
9. (Elimu na mafunzo ya ufundi) - Prof Jumanne Maghembe, Manaibu Gaudensia Kabaka , na Mwantum Mahiza.
10. (Mawasiliano, Sayansi na Technologia) - Shukuru Kawambwa, Naibu Maua Daftari.
11. (Miundo mbinu) - Andrew Chenge, Naibu Milton Mahanga.
12. (Habari Utamaduni na Michezo) - George Huruma Mkuchika, Naibu Joel Bendera.
13. (Kazi Ajira na maendeleo ya Vijana) - Prof Juma Kapuya, Naibu Ezekiel Chibulunje.
14. (Maji na Umwagiliaji) - Prof. Mark Mwandosya, Naibu wake ni Engineer Christopher Chiza. 15. (Kilimo Chakula na Ushirika) - Prof. Peter Msola, Naibu Mathayo David Mathayo.
16. (Maendeleo ya jamii Jinsia na Watoto) - Magreth Sitta, naibu Lucy Nkya.
17. (Maendeleo ya mifugo na uvuvi) - John Pombe Magufuli, Naibu DR. James Wanyancha.
18. (Maliasili na utalii) - Shamsa Mwangunga, Naibu Ezekiel Maige.
19. (Mambo ya Ndani) - Lawrence Masha, naibu Hamis Kagasheki.
20. (Wizara ya Katiba na Sheria) - Mhe. Mathias Chikawe.
21. (Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa) - Bernard Membe, naibu Seif Ally Idi.
22. (Wizara ya Nishati na madini) - Wiliam Ngereja, Naibu ni Adam Malima.
23. (Wizara ya Ulinzi) - Hussein Ally Mwinyi, Naibu Emmanuel Nchimbi.
24. (Wizara Ya Afrika Mashariki) - DR. E Kamala, naibu Mohamed Abdul.
25. (Viwanda na Masoko) - Mary Nagu naibu Cyril Chami.
Wameisha!!!!!!

Thursday, 7 February 2008

BREAKING NEWS!!!!!

Mh.. EDWARD LOWASA (PM)


HABARI TOKA DODOMA SASA HIVI ZINASEMA KUWA SPIKA WA BUNGE MH. SAMWEL SITTA AMETANGAZA KWAMBA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA AMEAMUA KUJIUZULU UWAZIRI MKUU.


MH. SPIKA BAADA YA KUTANGAZA HILO AMESEMA MJADALA WA RIPOTI YA RICHMOND, NA SIO MJADALA WA LOWASSA, NDIO UENDELEE. NA NDICHO KINACHOFANYIKA HIVI SASA HUKO BUNGENI.


HABARI ZAIDI ZINASEMA KWAMBA MH. LOWASSA AMESEMA KWAMBA INGAWA HAJAMTAARIFU JK UAMUZI WAKE HUO, AMEAMUA KUJIWEKA KANDO.


PIA AMEWAELEZA WAANDISHI WA HABARI KWAMBA KAMATI HIYO IMELIAMBIA BUNGE UONGO KWA KUTUMIA ZAIDI MANENO YA UZUSHI. MHESHIMIWA HUYO PIA AMEWEKA BAYANA KWAMBA MPAKA SASA HAJUI NI NANI HASWA ATACHUKUA NAFASI YAKE KAMA RAIS ATARIDHIA OMBI LAKE LA KUJIUZULU WADHIFA WAKE.
BUNGE LIMEAHIRISHWA MPAKA JIONI YA LEO SAA 11 KWA MAAMUZI ZAIDI!
NAWAKILISHA!

Wednesday, 6 February 2008

Mambo ya RICHMOND hayooooooo!!!





Jengo jipya la Bunge Dodoma


Haya sasa ile ripoti ya ubadhilifu wa mamilioni ya fedha za walalahoi sakata la Richmond hii hapa!
Kong'oli hapa http://watanzaniaoslo.blogspot.com/.

Monday, 3 December 2007

ADA YA KILA MUHULA

Salamu kwa wote!

Mnakumbushwa kuhusu kuwakilisha ada za uanachama za kila muhula kwa mhazini wetu. Kama hutaweza fanya hivyo, waweza mpatia kiongozi yeyote na mchango wako utafika mahala unapohitajika kufika.

Ada ni 200NOK

Ahsante kwa ushirikiano wako!

Mhazini - TASAO

Friday, 9 November 2007

INVITATION

Reception and Meeting with Zambia’s Former President

Dr. Kenneth D. Kaunda


Wednesday 14 NOVEMBER 1800 – 1930
Voksenåsen Oslo
Ullveien 4, 0791 Oslo
http://www.voksenaasen.no/

K.K. Is coming to Norway to attend an international conference:

“A Dialogue conference on the unpredictable past and future of genocide,”

which is to be held at Voksenåsen November 16 and 17. To mark this occasion, Voksenåsen in collaboration with Networkers South North is hosting a reception and meeting with Dr. Kenneth D. Kaunda.

One remembers Kenneth David Kaunda for his important role in the fight against colonial powers, apartheid in Southern Africa throughout several decades of the 20th century. Kenneth Kaunda is 83 years old and is still active both in political diplomacy and in the fight against HIV/AIDS.

It is crucial that guests RSVP by Sunday, November 9 to confirm their attendance to the of the following email address:

bagandatz@yahoo.co.uk.

Food and Drinks will be served for free!!!!


On Behalf of Networkers and Voksenåsen

Karl Einar Ellingsen and Øystein Tveter

Tuesday, 16 October 2007

'Sex Play' in kindergartens - Watanzania mpooh!!


Norwegians woke up Tuesday morning to news that a respected Oslo pre-school teacher, backed by child psychologists, thinks children should be allowed to openly express their own sexuality, not least through sex play and games in the local day care centers known as barnehager, or kindergartens.

The vast majority of Norwegians send their children from the age of one to the kindergartens, where they spend their days until they begin school at age six.

Pia Friis, leader of the popular Bjerkealleen Barnehage in Oslo and a well-known pre-school educator, told newspaper Dagbladet on Tuesday that children should be allowed to express their own sexuality at day care centers. She doesn't want to stifle what comes naturally.

Children, she said, should be able "to look at each other and examine each other's bodies. They can play doctor, play mother and father, dance naked and masturbate.

"But their sexuality must also be socialized, so they are not, for example, allowed to masturbate while sitting and eating. Nor can they be allowed to pressure other children into doing things they don't want to."Friis said there's a lot of uncertainty around how day care center employees should handle children's sexuality.

"The only thing that is absolutely certain is that children, sooner or later, will play sexual games and examine each other at the kindergarten," she told Dagbladet. "When the personnel are uncertain, that passes on to the children, and it can be negative."

The issue is the topic of an article in the latest edition of the magazine published by Norway's industry association for privately owned kindergartens, PBL-nytt, and Friis thinks it's important. So do child psychologist Thore Langfeldt and family therapist Jesper Juul. "Children must learn about sexuality, otherwise things can go very wrong," said Langfeldt. "Children can't object to something they don't know about, and children can more easily and readily report assaults if they already are aware of their own sexuality." Juul conceded that "many are disturbed by children's sexuality, but I think it's important to put it on the agenda. That, in fact, is what we're doing."

While Norwegians are known for being liberal and tolerant, the issue already has sparked heated debate on radio programs and in online opinion forums. And some politicians are outraged, not least those on the conservative side. "I thought at first that this was a joke," said Karin Ståhl Woldseth, a spokesman on family issues for the Progress Party.

"Sexual games don't belong in a kindergarten," she declared. "Children don't need more exposure to this in kindergartens. We think it will damage their health."


Source: Aftenposten English Web Desk

Wednesday, 5 September 2007

SHUKRANI KWA FARAJA ZENU

Hi TASAO!


Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wote kwa kunifariji katika kipindi hiki kigumu cha kufiwa na mama yangu mzazi ambaye aliaga dunia tarehe 07.08.2007saa tano usiku ghafla, nawashukuru wote kwa mkono wa pole na nawaombea kwa mwenyezi mungu awazidishie saba mara sabini.
Sisi tulimpenda sana mama yetu mpendwa lakini mungualimpenda zaidi, jina lake lihimidiwe na mungu ailazemahali pema roho ya mama yetu mpendwa.
Nawatakia wote masomo mema na kazi njema, mwenyezi Mungu awatangulie katika kila jambo mnalofanya.

Mzee wa mawe,

James Apolkarpi

Mob#: +255 754 588706

Email: james2001tz@ yahoo.com
03.09.2007

Tuesday, 7 August 2007

Kwa wanaopenda kujiendeleza kielimu!

MSc & PhD study opportunities in Norway!

The government of Norway provides sponsorship to over 500 students from the developing world for Masters and PhD programs at various 46 Universities/ colleges in Norway every year. Experience shows that Tanzania get 50 positions (over 10%) of these places since most of Tanzanians go back after completing their studies.

1. All Tanzanians who are interested are called to apply. AtNIMR there are opportunities for Scientists and other staff. See the list of 46 Universities below. I have to say that please let as many people you know as possible apply (even outside of NIMR) - as most people may not have this information. In each University, there are procedures for application -the web page in Norwegian (click English) - to see the info in English. Then go to prospective students, then choose Quota program then make two choices. Initially you will fill in preliminary appl. - then they will send you the appl. forms through email.

2. Academic requirements: Basic training with General Pass Average (GPA) of 3.5 (Upper Second) and above - those with 1st Class usually are selected as policy. In addition, indication of Work experience is important. (Not mandatory as there are many Masters’ students studying here just fresh from Schools in Tanzania.

3. Sponsorship: These programs are fully sponsored. Education in Norway is free- so no tuition fees! The government will give you stipend to support food, travel accommodation etc. There are three main sponsorship arrangements:
I. Quota- this is the largest-
II. NOMA (formerly NORAD) - this is mainly for Masters and students do their studies either in South Africa or Makerere – Uganda but get funds as if they are studying in Norway.

4. Deadline for Application is 1st of December. All application forms together with letters of support, original certificates and other information should reach the Universities by this date.

5. Best places for NIMR Scientists/ Support staff.
i. University of Bergen
ii.University of Oslo
iii.University of Trøndheim
iv.University of Trømso

For Administrators at NIMR- Masters of Public Administration in Bergen and Oslo are very good courses- there are students from Mzumbe, from Uganda, Ghana etc.

6. PhD Program requirements: A protocol addressing priority problems is needed. From experience- Universities in Norway don’t accept other Masters from other countries for PhD directly- you will need one year to be assessed for Masters and in the second year you can switch to PhD program. If you have Masters in Norway you will be accepted directly- PhD prog. is three years- If you have Masters from elsewhere PhD prg. is 4 years. In the PhD prog. while studying in Norway req. is publication of 3 or 4 articles in peer reviewed journals.

7. If you are interested- or you have relative or friend, someone you know, with good qualifications- please pass the info. If you are unable to get the forms- feel free to contact TASAO or any Tanzanian student studying in Norway.

We encourage as many Tanzanians as possible to apply!

Academic institutions in the Quota Scheme
1. Universities Norwegian University of Life Sciences http://www.umb.no/
2. Norwegian University of Science and Technology http://www.ntnu.no/
3. University of Bergen http://www.uib.no/
4. University of Oslo http://www.uio.no/
5. University of Stavanger http://www.uis.no/
6. University of Tromsø http://www.uit.no/
7. National academies of the arts Bergen National Academy of the Arts (KHIB) http://www.khib.no/
8. Oslo National Academy of the Arts (KHIO) http://www.khio.no/
9. Akershus- http://www.hiak.no/
10. Bergen http://www.hib.no/
12. Buskerud http://www.hibu.no/
13. Finnmark http://www.hifm.no/
14. Gjøvik http://www.hig.no/
15. Harstad http://www.hih.no/
16. Hedmark http://www.hihm.no/
17. Lillehammer http://www.hil.no/
19. Narvik http://www.hin.no/
20. Nord-Trøndelag http://www.hint.no/
21. Oslo University College http://www.hio.no/
23. Sogn og Fjordane http://www.hisf.no/
24. Stord/Haugesund http://www.hsh.no/
25. Sør-Trøndelag http://www.hist.no/
26. Telemark http://www.hit.no/
28. Vestfold http://www.hive.no/
30. Østfold http://www.hiof.no/
31. Ålesund http://www.hials.no/
32. Barratt Due Institute of Music http://www.barrattdue.no/
33. Bergen Deaconess University College http://www.bergendsh.no/
34. The Norwegian Academy of Music http://www.nmh.no/
35. The Norwegian School of Economics and Business Admini stration http://www.nhh.no/
36. The Norwegian School of Veterinary Science http://www.veths.no/
37. The Norwegian University of Sport and Physical Education http://www.nih.no/ (Wamesitisha zoezi la kuchukua wanafunzi kwa mwaka huu)
38. The Norwegian School of Management http://www.bi.no/
39. The Norwegian College of Eurytmy http://www.eurytmi.no/
40. The Norwegian School of Theology http://www.mf.no/
41. The Norwegian Teacher Academy http://www.nla.no/
42. The Oslo School of Architecture and Design http://www.aho.no/
43. Queen Maud`s College http://www.dmmh.no/
44. Rogaland College - http://www.diakonhjemmeths.no/
45. The Rudolf Steiner College of Education http://www.rshoyskolen.no/
46. The School of Mission and Theology http://www.mhs.no/

Monday, 18 June 2007

SHEREHE MAALUM YA KUWAAGA WANA TASAO WANAOREJEA NYUMBANI BAADA YA MASOMO YAO - 30.04.2007