Friday 2 March 2007

Taarifa ya kikao cha TASAO tarehe 24.02.07

1. Kikao kilifanyika

Tarehe: 24-02-07
Mahali: Chuo kikuu cha Sayansi ya michezo na elimu ya viungo-Norway (NIH) -Songsvann

2. Kufunguliwa kwa kikao
Kikao kilifunguliwa rasmi na aliyekuwa mwenyekiti wa muda wa TASAO.


3. Kusomwa kwa taarifa ya kikao kilicho pita.
Katibu alisoma taarifa ya kikao kilicho tangulia cha tarehe 03-02-07.
Wanachama walikubaliana na taarifa hiyo.

4 Yatokanayo na kikao kilichopita.
Kikao kilichopita kilidhamiria pamoja na agenda nyigine, kufanya uchaguzi kwa mujibu wa katiba. Hivyo kilipendeleza tarehe 24-02-07 kuwa ndiyo situ ya ya uchaguzi mkuu wa TASAO.

5. Zifuatazo ndiyo zilikuwa agenda za mkutano
(i) Mahafali ya kuwaaga wanaomaliza
(ii) Ada ya uanachama
(iii) Ujio wa Rais Kikwete
(iv) Uhusiano wa TASAO na vyama vingine Norway
(v)Uchaguzi wa viongozi
(vi) Mengineyo

6. Mahafali ya kuwaaga wanaomaliza

Kikao kwa pamoja kilikubali kuwepo na mahafali ya kuwaaga wanaomaliza. Ili kuweza kuwaaga wote wanaomaliza kwa pamoja, wajumbe walipendekeza kufanya sherehe mapema. Kwa kuwa wanafunzi wanapishana muda wa kumaliza, ilionekana ni vema tufanye sherehe mwezi wa nne(April) na iwe situ ya ijumaa ili kuruhusu wajumbe kushiriki. Tarehe rasmi itatangazwa baadae.

7. Ada ya uanachama
Kikao kilitangaza rasmi kuwa kutakuwa na ada za aina mbili
(i) Ada ya kuingilia uanachama
Hii ni ada itakayokupa uhalali wa kuwa mwanachama wa TASAO
Kikao kilipitisha NOK 100/=
(ii) Ada ya kila semister
Kikao kiliona kuwa ili kuepusha michango ya mara kwa mara ni vema kuwa na mchango wa kila semester. Kwa pamoja walikubali kuchanga NOK200 kwa kila semister.
ANGALIZO:
Wajumbe walipendekeza kuwa ni vema matumizi na mapato ya TASAO yawekwe wazi kwa kila mwanachama.



8. Ujio wa Rais wa Tanzania.
Wajumbe kwa pamoja walijadili kuhusu ujio wa Rais Kikwete nchini Norway. Wajumbe kwa pamoja waliona kuna haja ya kuwa na risala yao kama wanafunzi kwa mheshimiwa Rais. Waliona kuwa risala yao igusie masuala ya wanafunzi wakiwa masomoni nje ya nchi na ndugu zao walio kule nyumbani Tanzania. Kwa hali hiyo, waliona kuna haja ya kuunda kamati ili kuweza kuandika risala yao kwa kupokea michango mbalimbali kutoka kwa wanafunzi. Kikao kilichagua wajumbe wawili. Wajumbe hao wataungana na Rais, Katibu na Makamu wa Rais watakaochaguliwa hapo baadae. Hivyo kamati ya kuandika risala ilikuwa na watu watano.

Wajumbe wafuatao walichaguliwa na mkutano
(i) Hafsa, Waziri
(ii) Robert, Ngukah

9. Uhusiano wa TASAO na vyama vingine vya Kitanzania hapa Norway
Mkutano uliona kuwa TASAO ni chama kipia na wengi hawajakifahamu. Kuna haja ya kukitangaza chama na watu waelewe malengo ya chama. Moja ya jambo alilosisitiza mwenyekiti ni kuwa lengo la TASAO ni kuendaleza ushirikiano na vyama vingine. TASAO pia iliona kuwa kuna haja ya kupanua ushirikiano na kuheshimu vyama vingine hasa vya Kitanzania hapa Oslo na Norway kwa ujumla

10. Uchaguzi wa viongozi
Ili kuweza kuendesha zoezi la uchaguzi, Kamati ya uchaguzi iliundwa. Wafuatao walichaguliwa
(i) Juma Lungo (M/kiti)
(ii)Kisa Mwakatobe (katibu)
(iii)Jacob Mwangomola (mjumbe)

Mara baada ya uchaguzi wa kamati ya uchaguzi, viongozi wa muda walivuliwa madaraka na zoezi la uchaguzi likaanza.

11. Matokeo ya uchaguzi
NO. Nafasi Jina
1 Rais wa TASAO John Chalukulu
2 Makamu wa Rais Blakson Kanukisya
3 Katibu TASAO Alice Makule
4 Mtunza Fedha Beatrice Chingumile
5 Academi&recreation i)Hezron Nonga ii)Inocent Buberwa
6 Heath Zawadi Kinyamagoha
7 Wajumbe kamati ya fedha Faraja Ingira, Mary Wariro
8 Wajumbe Amir Makame, Linda lugenge

12. Mengineyo
Rais aliwashukuru wanachama kwa kuwa na imani nae na alisisitiza ushirikiano kwa wana-TASAO

13. Kufunga kikao
Kikao kiliahirishwa hadi kitakapo tangazwa tena saa 11:32