Friday, 24 May 2013

Tanzania Mtwara gas riots: 'Pregnant woman killed'


 A house set alight in Mtwara, Tanzania in May 2013
Schools and businesses in Mtwara are closed because of the tensions
A pregnant woman has been shot dead in Tanzania during a security operation after protests in Mtwara, a journalist in the southern town has told the BBC.
The security forces were hunting for those thought to be behind the violent riots that erupted two days ago.
Residents were angered that the budget, presented in parliament on Wednesday, confirmed the construction of a gas pipeline from Mtwara to Dar es Salaam.
They want a gas processing plant to be built in Mtwara instead.
The 500km (310-mile) pipeline is part of a $1.22bn (£807m) project which will also see the construction of a gas processing plant in Dar es Salaam, the main city of the East African nation.
Map
Fleeing Journalist Abdallah Bakari, who works for Tanzania's privately owned Mwananchi newspaper, told the BBC Swahili service that the woman was shot in her home on Thursday.
The security forces were going house-to-house to search for people they thought had been involved in the clashes with police.
Dr Mohamed Kodi at Mtwara's Ligula Referral Hospital told Mwananchi that the woman who died was shot in the stomach. She was seven months pregnant, he said.
Her shooting was also reported in the Kiswahili-language paper Nipache.
The local police commander has refused to comment on the incident.
Correspondents say many men have fled the town because of the crackdown and some women and children have sought shelter in the grounds of Ligula Hospital for safety.

Burning tyres in Mtwara in Tanzania - May 2013 The riots began on Wednesday when the budget confirmed the gas project was going ahead.


When the riots broke out on Wednesday, some buildings and vehicles were set alight, cars were stoned and a bridge blocked to stop traffic.
Riot police were deployed and soldiers can now be seen patrolling the streets.
Police have been escorting buses travelling into Mtwara to stop them being attacked.
Shops, schools and other businesses in the town remain closed because of the tensions.
There were similar protests in January about the proposed pipeline when the houses of several governing party politicians were burnt down.
Parliament has been temporarily suspended because of the latest trouble.
But President Jakaya Kikwete has said the government will continue with the project despite the protests.
Their demands are not valid because resources belong to the whole country, not one geographical area, he said.

Source: BBC.Com

HALI BADO NI TETE MTWARA


Na Waandishi Wetu, Mwananchi  (email the author)

Posted  Alhamisi,Mei23  2013  saa 19:32 PM
Kwa ufupi
Magomeni A hatuna amani, askari wanaingia nyumbani kwetu, wanatupiga na kutunyang’anya simu, yaani huku Magomeni hatuna amani kabisa, tumepotezana na watoto na hatujui hata waume zetu wako wapi


Mtwara. Wakati mtu mwingine akiripotiwa kufa, hali bado ni tete katika Mji wa Mtwara kutokana na mabomu ya machozi na risasi za moto kuendelea kurindima kwenye mitaa kadhaa wakati polisi wakipambana na makundi ya vijana wanaopinga mradi wa ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi alithibitisha kupokea mwili wa mjamzito ukiwa na tundu tumboni, linaloaminika kuwa linatokana na risasi.
“Ni kweli kwa leo tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa miezi saba akiwa amepigwa risasi tumboni,” alisema Dk Kodi. Inadaiwa kwamba mjamzito huyo ambaye jina lake halikufahamika, ameuawa akiwa nyumbani kwake. Kifo hicho ni cha pili baada ya Karim Shaibu (22), mkazi wa Chikongola kuuawa juzi.

WOULD YOU LIKE TO BE A WRITER, AUTHOR OR COLUMNIST. HERE IS YOUR CHANCE

TASAO like other blogs, would like to invite anyone who is inspired in writing different social, cultural, economic and political issues . The most important thing is to ensure your writings does not create any conflict in terms of language used and remember to be sure of what you write and if possible site the source of information for evidence based facts.

It is very easy if you are ready for this motivation. Just write and send to us via our 
Email: studentsunion.oslo@gmail.com
All of your writings will be published here for the readers.
Thanks
PRO

Thursday, 23 May 2013

Askari-watuhumiwa-kubaka-kumwua-mjamzito-kupora-kuchoma-nyumba-moto

Picture
Askari wakiwa lindoni/doriani, Mtwara
Hali ya usalama katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani hapa imezidi kuwa mbaya baada ya askari polisi kudaiwa kufanya unyama kwa kuwabaka wanawake na kumpiga risasi mjamzito

Mbali na unyama huo polisi pia wanadaiwa kuchoma moto nyumba tatu za wananchi katika mtaa wa Magomeni na vibanda vya maduka kadhaa na kupora vitu vilivyomo ndani.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa anasema hali ni shwari na kwamba wananchi watoke nje kuendelea na shughuli zao kama kawaida.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi amethibitisha kupokea mwili wa mjamzito ukiwa na tundu tumboni, zinazoaminika kuwa za risasi na hivyo kufanya idadi ya maiti zilizopokelewa hospitalini hapo kufikia mbili na majeruhi 18: “Ni kweli kwa leo tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa
miezi saba, amepigwa risasi tumboni...” “...pia tumepokea mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Chuno, amevunjwa miguu yote kwa risasi.”

Habari zinadai kuwa mjamzito huyo ameuawa akiwa nyumbani kwake baada ya polisi kuvamia makazi yake.

Huduma za kijamii zimesimama, hakuna maduka yaliyo wazi, hakuna usafiri wa daladala wala pikipiki, mji upo kimya, sauti za milio ya mabomu na bunduki zimetawala, wanajeshi waliovalia sare wameuzingira mji wakiwa katika magari na pikipiki.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti wakazi hao wamelalamikia kitendo cha askari wa jeshi la polisi kuingia katika makazi yao, kuwapiga, kuwabaka na kuwapora mali zao:

“Magomeni A hatuna amani askari wanaingia majumbani mwetu wanatupiga na kutunyang’anya simu, yani huku Magomeni hatuna amani kabisa, tumepoteza watoto na hatujui hata waume zetu wako wapi” alisema Paulina Idd na kuongeza: “Majumba yetu yamechomwa moto wanaofanya fujo ni polisi wenyewe halafu wanakuja wanatubaka na kuiba mali zetu halafu tunateseka sisi yaani tumechoka kabisa na serikali yenyewe,” alisema Paulina.
Picture
Wanawake na watoto wakiwa hospitali ya rufaa ya Ligula, Mtwara kwa ajili ya kuomba hifadhi baada ya kuyakimbia makazi yao kwa hofu
Kamanda Sinzumwa alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa atapingana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Mchimbi aliyewasili Mtwara leo: “Kuhusiana na suala hilo siwezi kulizungumzia kwa sasa kwani nitapingana na Waziri wangu kwani leo ametoa tamko bungeni na leo atawasili,” alieleza Sinzumwa

Wakazi wakimbia maeneo yao
Wakazi wa maeneo mbalimbali wamekimbia makazi yao hususani wanawake na watoto na kuhamia hospitali ya rufaa kwa kuhofia usalama wao huku wengi wao wakipotezana na ndugu zao.

Hali hiyo imetokea kufuatia kuwepo kwa milipuko ya mobomu katika maeneo mbalimbali mjini hapa huku huduma za kijamii zikiwa bado zimesitishwa. Hali hiyo imetokea baada ya kusambazwa kwa vipeperushi vilivyokuwa vikihamasisha wananchi wa mkoani hapa kusitisha huduma zote hapo jana  ili kusikiliza hotuba ya wizara ya nishati na madini.

Kufuatia hali hiyo imesababisha kifo kwa raia mmoja aliyefahamika kwa jina Karim Shaibu (22) mkazi wa Chikongola ambaye alipigwa risasi wakati wa fujo kati ya jeshi la polisi na wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari mganga mkuu wa mkoa hospitali ya rufaa ya Ligula Dk Sadun Kabuma alithibitisha kupokea kwa kifo hicho ikiwa ni pamoja na majeruhi 17 wakiwemo askari watatu: “Ni kweli jana kuanzia majira ya saa 10 hadi saa 11 nilipokea majeruhi 17 ambapo kati ya hao wamishtuko ni wanawake watano na askari watatu na kijana mwingine ambaye alikuwa na jeraha na katika harakati zan kumwokoa maisha yake alifariki akiwa chumba cha upasuaji,” alisema Dk Kabuma

Wananchi wazungumzia bajeti

Wakizungumzia uwasilishwaji wa hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini wakazi wa hapa wamesema kuwa hawakubaliani na ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwani mpango huo utawaletea dhuluma: “Mpango wa kusafirishwa kwa gesi asilia hatuna mpango nao kwa wakazi wote wa Mtwara kwa kifupi akina mama wa mtwara hatutaki itoke,” alisema Fatuma Abdallah.

---
Imenukuliwa kutoka wavuti.com kwa msaada wa KARIBU KUSINI Blog

Source: http://www.wavuti.com/4/post/2013/05/mtwara-askari-watuhumiwa-kubaka-kumwua-mjamzito-kupora-kuchoma-nyumba-moto.html#ixzz2U8mSnwWA

Uhuru Day, Easter party, and Muungano PICTURES- Mixed Reactions


TANGAZO MUHIMU

Ndugu wanaTASAo kama ilivyo ada yetu ule muda wa kuwaaga wenzetu wanaomaliza masomo mwaka 2013 umewadia. Sherehe zitafanyika siku ya Jumamosi ya Tarehe 08.06.2013. Sherehe hizi zitafanyika katika Ukumbi wa NORGBERG KIRKE pale ilipofanyika sherehe ya Uhuru mwezi Desemba 2012. Sherehe zitaanza saa 12.00 jioni.

Tunaomba sana wote tushiriki kwa wingi.

Sambamba na hilo tunaomba kuwakumbusha michango ya Kiingilio na Ada ya kila muhula kwa wale ambao hawajatoa. Kwa sababu sherehe hizi zinaendeshwa kwa michango yaani Kiingilio na Ada tu hakuna mchango zaidi ya huo. Tunawaomba sana tujitume wenyewe. Unaweza wasilisha mchango wako moja kwa moja kwa kiongozi yeyote wa TASAO.

Naomba kuwasilisha.

Tunawasalimu pia wale wote mlio huko nyumbani Tanzania. Kila la kheri katika kujenga nchi yetu.
DEZIDERY KAJUNA
PRO

Thursday, 27 September 2012

MATUKIO KATIKA PICHA KUHUSU SIKU YA KUWAAGA WANATASAO WALIOMALIZA VYUO MBALIMBALI OSLO NA HAMAR 12.06.2012

Saturday, 22 September 2012

 Mhe Rais Godrick Lyimo kulia, katikati ni rais mstaafu Mhe Doreen Ndosi na kushutu ni Mchg Eilzabeth Silayo mwanafunzi Oslo University


KUHUSU KUWAKARIBISHA WANAFUNZI WAPYA KATIKA CHAMA CHA TASAO(TANZANIA STUDENT ASSOCIATION IN OSLO)

Tarehe 22/08/2012 jumuyia ya wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Oslo, Norway wamekuta na kuwakaribisha wanafunzi wapya waliokuja kusoma shahada mbalimbali.

Mhe Rais wa TASAO Mchg. Godrick Lyimo alichakuwa nafasi ya kuwakaribisha wanafunzi hao waliokuja masomoni mwaka huu wa wa masaomo 2012/13. Mhe. Rais aliwapongeza sana wanafunzi hao kwa kupata nafasi ya kuja kusoma Norway, nafasi ambayo sio kila mtu anapata, Mhe Rais pia aliwaambia wanafunzi wapya malengo na madhumuni ya kuwepo kwa chama cha TASAO kuwa ni kujenga umoja wa wanafunzi wa Kitanzania ili waweze kusaidiana wakati wa shida na wa raha, kukaa kama ndugu wakiwa nje ya nchi yao. Mhe Rais aliwaomba wanafunzi wote wapya na wa zamani waendelee kushikamana na kusaidiana kama ndugu maana Tanzania ni moja na watu wake ni wamoja.

Wednesday, 6 April 2011

Mkutano Mkuu wa TASAO na Uchaguzi wa Viongozi Wapya




Tarehe 1 Aprili, 2011 wanajumiya ya TASAO walifanya mkutano mkuu kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali yahusuyo jumuiya hiyo pamoja na kufanya uchaguzi wa viongozi wapya. Ilikuwa ni siku ya furaha sana kwa wana-TASAO walioweza kuhudhuria mkutano huo. Licha ya kuwa na shauku ya kuonana kama kikundi cha Watanzania baada ya miezi kadhaa, ilikuwa ni nafasi nzuri kwao kushirikishana juu ya mambo mbalimbali yanayojiri hapa Norway na hata kule nyumbani Tanzania, huku wakijipatia vinywaji baridi na vitafunwa. Suala la babu wa Loliondo anayegawa 'vikombe' vya tiba ya magonjwa mbalimbali lilivuta hisia za wajumbe, hasa wale waliofika dakika za mwanzoni, huku baadhi yao wakionesha wasiwasi juu ya uwezo wa tiba hiyo.

Baada ya kujadili agenda mbalimbali juu ya mafanikio na changamoto zinazoikabili TASAO, wajumbe wa mkutano walichagua viongozi wapya kwa ajili ya kukiongoza chama kwa kipindi cha mwaka 2011/2012. Yafuatayo ni majina ya viongozi wateule na vyeo vyao kwenye mabano: Ndg. Doreen Ndossi (Mwenyekiti), Ndg. Andrew Munisi (M/Mwenyekiti), Ndg. Janeth Mwakalinga (Katibu), Ndg. Michael Pima (Mhazini), Ndg. Ellance Mbilu (blog moderator).

Mwenyekiti mteule wa tume ya muda ya uchaguzi, Mch. Syprian Hilinti, aliwatangaza rasmi viongozi hao wapya na kuwataka wanachama wawape ushirikiano.

Friday, 31 December 2010

TAARIFA YA MSIBA

Habari watanzania wenzangu!

Nachukua nafasi hii kuwapa taarifa kuwa ndugu yetu Marcelin Raphael Ndimbwa amefiwa na baba yake mzazi huko Mbeya leo asubuhi saa 12. Taarifa zaidi za mazishi tutaendelea kufahamishana.

Hivyo tujumuike pamoja katika kumfariji mwenzetu kwa hali na mali na kumuombea ili aweze kumpumzisha salama baba yetu.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.

Amina!

Fatuma Hussein.

Thursday, 22 July 2010

Usafiri wetu ni ule ule, ila aina ya gari hubadilika kutokana na mazingia na hali ya barabara


Safari yangu ilikuwa ndefu sana, hapa Naingia Mbeya kutokea Tabora

Hivi ndivyo tunavyosafiri tukiwa makwetu, Bora kufika.

Thursday, 15 July 2010

Wanyamapori ni rasilimali kwa watanzania wote, lazima tuilinde

Enzi za Mababu: ukiwa porini unalazimika kuwasha moto kwa kupekecha vijiti. Hata tunakutana na mwenyeji wa pori hili, mzee wa kimasai na tunaomba kibiriti ili tuwashe moto. Jibu tulilopata hatukuamini, mara tukapewa moto kwenye fungu la kinyesi cha punda. Upekechaji ulichukua takribani dakika tano tu.

Sunday, 27 June 2010

HAVE YOU EVER VISITED RUAHA NATIONAL PARK? HERE ARE SOME CLUES

Ruaha National Park is the largest national park in Tanzania. Located in the middle of Tanzania about 130 km from Iringa, the park is part of a more extensive ecosystem which includes Rungwa Game Reserve, Usangu Game Reserve, and several other protected areas.
The name of the park is derived from the Great Ruaha River, which flows along its south-eastern margin and is the focus for game-viewing. The park is very rich in both Fauna and flora diversity and can be reached by car via Iringa. There is an airstrip at Msembe, park headquarters. Underhere are some wildlife diversity.
FROM THE MAIN PARK ENTRENCE, THIS IS WHAT YOU SEE


Friday, 11 June 2010

Bajeti ya Kilimo Kwanza

11th June 2010

  • Kodi zake kibao zafutwa
  • Za bia, sigara, magari juu
  • Petroli, dizeli zapona
Bajeti mpya ya mwaka wa fedha wa 2010/11.

Serikali imetangaza bajeti mpya ya mwaka wa fedha wa 2010/11 ambayo imejielekeza kusaidia zaidi wakulima na wafugaji kwa kuwaondolea kodi mbalimbali, lakini imeendelea na jadi yake ya kuongeza kodi kwenye bia, vinywaji baridi, mvinyo, pombe kali, sigara na usajili wa magari.

Akiwasilisha bajeti hiyo bungeji jana jioni, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mukulo, alisema ongezeko la kodi hizo ni la asilimia nane kiwango ambacho hakizidi mfumuko wa bei.

Katika bajeti hiyo, mafuta ya petroli na bidhaa zake zote kodi zake hazijaguwa. Hata hivyo kuna punguzo mafuta ya kuendesha mitambo kutoka Sh. 97 hadi 80 kwa lita.

Ongezeko la viwango hivyo na vile vya zamani kwenye mabano ni vinywaji baridi Sh. 63 kwa lita (Sh. 58) na bia inayotengenezwa na nafaka ya hapa nchini na ambayo haijaoteshwa Sh. 226 kwa lita (Sh. 209) wakati bia nyingine zote zimepanda kutoka Sh. 354 kufikia Sh 382 kwa lita.

Alisema mvinyo unaotengenezwa kwa zabibu inayozalishwa nje ya nchi kwa kiwango kinachozidi asilimia 25 itakuwa Sh. 1,223 kwa lita (Sh 1,132) na vinywaji vikali itakuwa Sh. 1,812 kwa lita (Sh. 1,678).

Kwa upande wa sigara, Mkulo alisema zile zisizokuwa na kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75 itakuwa Sh. 6,209 kwa sigara 1,000 (Sh. 5,749).

Kwa sigara zenye kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa hapa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, itakuwa Sh 14,649 (13,564).

Alisema sigara nyingine zenye sifa tofauti na hizo, itakuwa Sh. 26,604 kwa sigara 1,000 (Sh. 24,633).

Wakati huo tumbaku ambayo ipo tayari kwa utengezaji wa sigara itakuwa Sh. 13,436 kwa kilo (12,441 na ushuru wa cigar unabaki kuwa asilimia 30.

“Hatua hizi katika ushuru wa bidhaa kwa pamoja zinatarajiwa kupunguza mapato ya serikali kwa kiasi cha Sh. bilioni 20.042,” alisema.

Mkulo alisema serikali imesamehe kodi ya majengo kwa nyumba wanamoishi wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60, ambao hali zao kiuchumi haziwawezeshi kulipa kodi hiyo.

“Hata hivyo msamaha huo utatolewa kwa wale watakaothibitishwa na uongozi katika serikali za mitaa kuwa kweli hawana uwezo wa kulipa kodi husika,” alisema.

Pia alisema kiwango cha kutoza ushuru wa mazao shambani kitakuwa kati ya asilimia 3 na 5 ya bei ya kuuza mazao mashambani, ili kuzipa fursa halmashauri na serikali za mitaa kutoza ushuru huo kulingana na uwezo na rasilimali zilizopo.

Ada ya usajili wa magari na pikipiki

Alisema usajili wa magari unatapanda kutoka Sh. 120,000 hadi Sh. 150,000 wakati pikipiki itakuwa Sh. 45,000 ikilinganisha na Sh 35,000 za awali.

Mkulo alisema hatua hizo zitaongeza mapato ya serikali kwa Sh. bilioni 3.19

Ada ya mwaka ya leseni

Kwa upande wa ada ya mwaka ya leseni za magari itakuwa Sh. 50,000 badala ya Sh. 30,000 kwa gari lenye ujazo wa injini 0-500cc.

Gari lenye ujazo wa injini 501 hadi 1,500cc, itapanda kutoka Sh. 50,000 hadi kufikia Sh. 100,000 wakati lenye ujazo wa kati ya 1501-2,500 itakuwa Sh 150,000 badala ya Sh 100,000.

Kwa upande wa gari lenye ujazo wa injini zaidi ya 2,501 ada itakuwa Sh 200,000 badala ya Sh. 150,000 ya sasa.

“Hatua hizi katika kuongeza viwango vya ada ya mwaka ya leseni za magari kwa pamoja zinatarajiwa kuongeza mapato ya serikali kwa kiasi cha Sh. bilioni 16.981,” alisema.

Usafirishaji korosho

Mkulo alisema kutakuwa na ongezeko la ushuru wa kusafirisha korosho ghafi kutoka asilimia 10 ya sasa hadi 15 (ama Dola 160 za Marekani) kwa tani moja.

Alisema lengo la ongezeko hilo ni kulinda viwanda, kuongeza ubora na thamani ya korosho na kukuza ajira kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Mkulo hatua hiyo inatarajiwa kuongeza mapato ya serikali kwa Sh bilioni 2.613.

Michezo ya kuhabatisha

Mkulo alisema kiwango cha kodi inayotozwa kwenye mashine za michezo ya kubahatisha itaongezeka kutoka Sh. 16,000 hadi 32,000 wakati kodi ya kiwango cha asilimia 13 ya mapato itatozwa katika mashine ya tombola, hivyo kuongeza mapato ya serikali kwa Sh. bilioni 0.5.

Misamaha wa kodi

Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka shambani hadi kwenye viwanda vya usindikaji kwa wakulima wenye kilimo cha mkataba wa miwa, mkongwe na chai imesamehewa.

Kodi nyingine iliyosamehewa ni VAT katika mashine na vifaa vya vya kukusanya, kusafirisha na kusindika maziwa ili kuhamasisha uwekezaji katika sekta ndogo ya maziwa na kuboresha kipato kwa wananchi.

Mashine na vifaa vitakavyohusika katika msamaha huo ni vifaa maalum vya kubebea maziwa, pampu maalum za kusukumia maziwa na bomba maalum la kupitishia maziwa kwenye viwanda vya usindikaji.

Vifaa vingine vilivyopata msamaha huo ni kompresa maalum zinazotumika kwenye vifaa vya kupoza maziwa, matanki ya kuhifadhia maziwa gari maalum lenye kifaa cha kupoza na kusafirisha maziwa.

Vingine ni mtambo maalum wa kuchemsha maziwa ili kutoa siagi, vifaa maalum vya kupoza na kutengeneza ubaridi na kifaa maalum cha kukandamiza na kukamua maji ili kuzalisha jibini.

Mkulo alisema msamaha mwingine umetolewa kwenye mashudu kwa ajili ya chakula cha mifugo.

Hatua hiyo inalenga kuhamasisha ufugaji bora na kuwawezesha wakulima wa mbegu za mafuta kupata bei yenye tija kwa mauzo ya bidhaa hiyo.

Pia, serikali imetoa unafuu maalum wa VAT kwa vifaa vinavyouzwa kwa watalaam wa mifugo waliosajiliwa.

Vitu vingine vilivyosamehewa VAT ni zana za kilimo kama kivuna nafaka, pick up balers, mashinde ya kufunga majani ya ng’ombe (hay making machinery) na mowers vinavyotumika mahsusi katika uzalishaji wa kilimo na mifugo.

Sekta ya kilimo cha maua nayo imenufaika na msamaha wa VAT kwa ufarishaji wa maua kwa ndege kwenda nje ya nchi, kwa mabanda (green house) yanayotumika katika kilimo cha maua.

Bajeti hiyo inaonyesha pia kutoa unafuu maalum wa VAT katika uuzaji wa bidhaa na huduma zinazotolewa kwa wakulima waliosajiliwa ama mashamba ya vyama vya ushirika na ujenzi wa miundombinu ya mashamba.

Miundombinu hiyo ni pamoja na mitaro ya umwagiliaji, barabara za mashambani, ujenzi wa maghala au huduma nyingine zinazofanana na hizo.

Pia msamaha wa VAT umetolewa kwa huduma za kuzalisha mifugo kwa njia ya kupandisha mifugo na kutumia mashine maalum za kuzalishia ama kutotolea vifaranga.

Mkulo alisema ili kuhamasisha uwekezaji na uzalishaji katika sekta ya viwanda nchini, unafuu maalum wa VAT umetolewa kwa waendelezaji wa maeneo yenye uwekezaji kwenye bidhaa za kuuza nje yaani EPZ na SEZ.

Mkulo alisema kutakuwa na tozo la VAT kwa asilimia sifuri katika usindikaji na uzalishaji wa mafuta ya kula kwa wazalishaji wanaotumia mbegu za mafuta zinazozalishwa hapa nchini.

Alisema VAT imesamehewa katika vifungashio vya juisi za matunda na bidhaa za maziwa.

“Hatua hii inalenga katika kupunguza gharama za uzalishaji na kuboresha thamani ya bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda vya juisi na maziwa hapa nchini,” alisema.

Mkulo alisema serikali imerejesha utaratibu wa kutambua baadhi ya vifaa kama bidhaa za mtaji kwa wawekezaji ili kuvipa nafuu ya kodi.

Hata hivyo, alisema serikali itaunda kamati maalum ya kushughulikia suala hilo, ili kudhibiti matumizi mabaya ya utaratibu huo yanayoweza kuvujisha mapato.

Alisema hatua hizo zinazohusu VAT zitasababisha kupungua kwa mapato ya serikali kwa kiasi cha Sh. bilioni 2.39.

Kuhusu sheria ya kodi ya mapato sura 332, Mkulo alitoa kauli ya kurekebisha kifungu cha 11 cha sheria hiyo ili kuweka wigo wa ukomo wa maeneo ya uchimbaji wa madini.

Alisema nia ni kudhibiti gharama zinazotakiwa kutolewa katika kukokotoa faida, itakayotozwa kodi ya mapato kwa eneo husika.

Pia kutokana na kuwepo biashara nyingi zinazofanywa na watu wasiokuwa na namba za utambulisho wa mlipa kodi (Tin), alipendekeza kodi ya zuio inayozuiwa na serikali kwa wauzaji wa bidhaa na watoa huduma wasiokuwa na Tin, izuiwe.

Mkulo alitangaza punguzo la ushuru wa bidhaa kwenye mafuta mazito ya kuendesha mitambo kutoka Sh. 97 hadi 80 ili kupunguza gharama za uzalishaji wa bidhaa hapa nchini.

Alisema hatua hiyo imezingatia ridhaa ya serikali kukuza viwanda, ajira na mapato ya ndani.

Pia alisema punguzo hilo limezingatia makubaliano ya serikali na wenye viwanda kupunguza ushuru huo na hatimaye kuufuta katika kipindi cha miaka mitatu.

Waziri huyo aliomba Bunge liidhinishe Sh. milioni 11,609,557 kati ya hizo matumizi ya kawaida ni Sh. milioni 7,790,506 na za maendeleo ni Sh. milioni 3,819,051.

CHANZO: NIPASHE

Monday, 7 April 2008

MKUTANO MKUU KATIKA PICHA - 29.03.2008

Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa TASAO, 2008 katika picha:

Sehemu ya Wajumbe wa mkutano

Wasimamizi wa uchaguzi wakitoka mkutanoni

Uchaguzi ukiendelea

Wasimamizi wa uchaguzi wakisoma taratibu za uchaguzi

Baadhi ya wajumbe wa mkutano

Baadhi ya wajumbe wa mkutano

BAADA YA MKUTANO MKUU

Mkutano mkuu ulifanyika vizuri na kwa mahudhurio ambayo kwa kweli yaliridhisha sana. Kwa kifupi agenda zote zilijadiliwa vizuri na kukubaliwa na wajumbe.

Baadhi ya maamuzi ya msingi ni:
1. Tarehe ya mahafali ya kuwaaga wanaomaliza muda wao wa masomo ilikubaliwa iwe ni: 9.may.2008

2. Uchaguzi wa viongozi wapya. Wafuatao walichaguliwa kuwa viongozi wa TASAO kwa mwaka 2008/2009

Nafasi Majina
Rais - John Chaluklu
Makamu - Rais Rose Matete
Katibu - Jane Bakahwemama
Mweka hazina - C. Lwiza
Accademic+ Recreation - Ernest Mjigo na Br. Nikuli
Afya na Ustawi - Said Bakari na Stela Bitanyi
Wajumbe Kamati ya fedha - Beatrice Chinguwile, Jelly Jerry
Wajumbe TASAO - Hezron Nonga na Julitha John

Uongozi uliotangulia unawshukuru wajumbe wote kwa ushirikiano wenu na unawaomba muendeleze ushirikiano zaidi kwa viongozi wapya!