
 Kama ni mfuatiliaji mzuri wa kipindi cha Skonga, utamkumbuka Happiness 
Watimanywa, msichana pekee kutoka Tanzania aliyeweka historia ya 
kuongoza nchi zaidi ya 150 za mtandao wa IGCSE katika somo la Uhasibu 
kwenye mitihani ya kidato cha nne mwaka 2010.
Happy
 (19) ni mzaliwa wa familia ya kawaida sana ya Mr Louis Roussos ya 
Morogoro. Wadogo zake Angel na Romeo sasa wanasoma St. Constantine shule
 iliyomtoa Happy. Pia, Happiness Watimanywa amewahi kusoma Laureatte 
International School ya Dar-es-salaam, ambapo akiwa hapo, alikutana na 
mwalimu wa michezo Mr Tchalewa Ndeki ambaye alimfungulia mipaka mingi 
Happy. Akiwa Laureatte, Happy aliwahi kwenda China na South Korea akiwa 
na wanafunzi wenzake katika matamasha mbali mbali ya elimu na michezo. 
Baada ya kumaliza kidato cha nne, Happy alifanikiwa kujiunga na Chuo 
Kikuu cha Strathclyde cha UK ambapo anasomea digrii ya Biashara.
Kipindi
 ambacho Happy yupo kwenye likizo ndefu, alipata wakati mgumu wa 
kutokuwa na kitu cha kufanya, hivyo Happy aliamua kujihusisha na masuala
 ya urembo na kufanikiwa kutwaa Taji la Miss Dodoma, na Miss Kanda ya 
Kati na hatimaye kuingia kwenye kambi ya Miss Tanzania. 
Akiwa
 Miss Tanzania, Happy alikuwa ni mshiriki wa kwanza kuingia Nusu Fainali
 ya mashindano hayo kwa kutwaa taji la Redds Miss Photogenic 2013.
Ndani
 ya kambi ya Miss Tanzania, Happiness Watimanywa amekuwa mwiba kwa 
warembo wengine 29 wanaowania taji hilo kwani amekuwa akionesha uwezo wa
 hali ya juu kuanzia kwenye kipaji hata michezo, ukiachilia mbali upeo 
mkubwa alio nao
SOURCE: FULL SHANGWE
HABARI ZAIDI TEMBELEA: http://othmanmichuzi.blogspot.no/2013/09/happiness-watimanywa-ndie-redds-miss.html





