Monday 19 August 2013

Muhimbili yawa na kitengo cha kurembesha watu

      

Madaktari wakimfanyia mtu upasuaji wa kurekebisha ukubwa wa titi 
Na Vicky Kimaro, Mwananchi  (email the author)

Posted  Agosti17  2013  saa 14:14 PM
Kwa ufupi
Inawezekana hufurahii umbo ulilozaliwa nalo. Kama ndivyo sasa teknolojia hiyo tayari imeingia nchini.


Miaka ya hivi karibuni, kumeibuka wimbi kubwa la wanawake kwa wanaume ambao wanafanyia matengenezo maumbile yao ‘Plastic Surgery’ kama sura, kupunguza vitambi, kuongeza makalio, kuongeza au kupunguza matiti.
Awali wimbi hili lilibuka zaidi kwenye nchi za magharibi, lakini kutokana na utandawazi, dunia kuwa kijiji, kwa hivi sasa watu wengi wamekuwa na mwamko wa kutengeneza shepu katika sehemu mbalimbali za maumbile yao.
Kwa hapa Tanzania, watu wengi hukimbilia nchini India kwenda kufanya upasuaji wa aina hii ambao wengi wao wanafanya aidha kwa kujua au kwa kutokujua madhara yake, lakini lengo kuu ni kujipendezesha na kuonekana mwenye mvuto machoni mwa watu.
Dk Zaituni Sanya bingwa wa upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili alifanya mahojiano maalum na Mwandishi wa habari hizi na kusema: “Kwa hapa Tanzania upasuaji unaofanyika ni ule wa kurekebisha sura na ule wa matiti ndiyo sana.”alisema
Akifafanua zaidi alisema: “Kwa upande wa sura upasuaji tunaofanya ni kwa wale ambao utakuta wameota vinyama au wana uvimbe uvimbe kwenye sura, ndiyo tunawafanyia na tena upasuaji wake unatumia nyuzi nyembamba sana maalumu ambazo hazionekani, lakini ule wa kuchonga sura kama ule uliokuwa ukifanywa na kina Michael Jackson hatufanyi.
“Upasuaji wa matiti ndiyo tunafanya sana hapa nchini, mimi binafsi ninafanya na kwa hapa Muhimbili gharama zake ni zilezile kama za upasuaji mwingine wowote, lakini kwenye hospitali za binafsi upasuaji huu ni gharama sana.
“Wengi wanaokuja hapa unakuta niwasichana kuanzia umri wa miaka 20 hadi 35 na hawa wanakuja siyo kwamba wanaumwa la hasha, wanafanya upasuaji huu kwa ajili ya urembo tu, unakuta matiti yao ni makubwa hivyo wanakuja kwa lengo la kuyapunguza.
“Matiti makubwa yanasababishwa na chembe chembe ambazo zinatengeneza mafuta na kuyafanya kuwa makubwa kupita kiasi, tunapofanya upasuaji tunaondoa mafuta yaliyozidi na kuliweka titi kwenye umbo zuri ambalo mhusika atataka na kwa saizi ambayo atapendelea, na pia wakati wa kushona inabidi uangalifu sana ili isisababishe madhara.
Mbali na kupunguza wanaongeza?
“Kwa hapa Tanzania hapana, toka nimeingia kwenye udaktari wa upasuaji mwaka 2004 sijapata mgonjwa ambaye anahitaji kuongeza ukubwa wa matiti zaidi ni kuyapunguza, na hii si tu kwa hapa Muhimbili bali pia kwenye hospitali kubwa zote za watu binafsi hakuna wagonjwa wa aina hii zaidi ya wale wanaohitaji kupunguza.
Hata hivyo Dk Sanya alisema kuwa hana takwimu sahihi za idadi ya watu ambao wanaenda kwa ajili ya tatizo hilo zaidi ya umri ambao wengi wao ni wasichana kati ya miaka 20 hadi 35.
“Upasuaji wa kupunguza matiti hauna madhara yoyote kwa vile tunapunguza chembe chembe zilizozidi pamoja na mafuta na hatutumii kemikali zozote. Ila kama upasuaji wake utakosewa basi madhara ambayo muhusika atapata ni kuwa hatoweza kumnyonyesha mtoto na kama mnavyojua matiti yakijaa misuli inapanuka na hivyo ni lazima mhusika atapata maumivu makali ambayo yatatibiwa na dawa za kutuliza maumivu.

“Kansa ni ugonjwa unaotokea tu kutokana na mfumo wa maisha na vyakula tunavyokula, lakini upasuaji huu wa kupunguza matiti hausababishi kansa, na maziwa mtoto asiponyonya kwa siku kadhaa ‘automatic’ yatakauka yenyewe ndiyo maana hata mama anayenyonyesha akiacha kumnyonyesha mtoto kwa wiki moja, mbili maziwa yanakauka.
“Ila kwa wale wanaongeza ukubwa wa matiti kuna madhara makubwa na si maziwa tu hata wale wanaongeza hipsi na makalio kwa kuwa ufanyaji wake unatumia kemikali... “Kitu chochote ambacho ni ‘artificial’ kina madhara na madhara makubwa ya kemikali zinazotumika kuongeza maziwa, hipsi na makalio ni saratani kwa kuwa ngozi ni ‘delicate’.
“Watu wanaofanya upasuaji huu kwa ajili ya urembo lazima watakuwa wanatumia maisha yao yote (medication) hali hii ni kujilimbikizia dawa mwilini, mwisho wa siku anajiua mwenyewe kama ilivyotokea kwa Michael Jackson.
WANAWAKE WANASEMAJE
Rhoda Sanga: Yawe makubwa yenye mvuto siyo pwaaa kama yanataka kumwagika, ukiwa na makubwa yaliyokaa vizuri unavutia zaidi ya yule mwenye vinyonyo vidogo.
Aisha Ally: Wengine wanatumia matiti kuvutia wanaume, wengine wanapenda tu jinsi yanavyowavutia na wengine tunapenda kumfurahisha mume na kupenda jinsi tu yalivyo, na ukiwa na ulapa lazima uongeze ‘sponge’ yavimbe.
WANAUME WANASEMAJE?
Henry Masanja: “ Wanawake wamegundua wanaume ndiyo wanapenda, na ni kweli tunapenda na yanatumika kwa staili nyingi, maziwa makubwa yana mvuto wa kimahaba na kimuonekano tofauti na mwenye maziwa madogo.
Allan Masawe: “Napenda makubwa yaliyosimama yamejaa siyo kandambili (yaliyolala) yanashikika, yanaongeza mvuto katika masula ya kimapenzi, unaweza maliza haja zako.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la Uingereza,mama mmoja mwenye umri wa miaka 46 anakumbuka namna alivyokaribia kupoteza maisha kutokana na matumizi ya dawa kwa ajili ya kufanyia marekebisho baadhi ya viungo vyake vya mwili, kwa nia ya kujipendezesha zaidi.
Apryl aliyetumia muda wake mwingi wa ujana kuremba nywele zake akizipaka dawa za aiana mbalimbali sasa anajuta.
Akiwa na kiu ya kurembesha mwili wake na kuwavutia wale wanaokatiza mbele ya macho yao, Apryl alichukua jukumu la kuongezwe vikorombwezo kwenye baadhi ya viungo vyake. Sasa akiwa na umri wa miaka 46, mwanamke huyo anatoa sauti ya masikitiko huku akiwaonya wengine kutofuata mkondo wa maisha aliyopitia.

Anasema kuwa amelazimika kujitokeza hadharani na kuelezea historia ya maisha yake, ili iwe funzo wa wengine wenye kiu kama aliyokuwa nayo awali. Anasema kuwa hakuwa na ufahamu wa kutosha juu ya kile alichokwenda kukifanya kama kingeweza kuvuruga kabisa amani na mwonekano wake aliojaaliwa na Mwenyezi Mungu.
Maisha yake kwa sasa ni ya wasiwasi na wakati mwingine anatakiwa kuwa mwangalifu mkubwa juu ya vyakula anavyokula, kutokana na kile kinachoelezwa kwamba ni mabadiliko ya kijenetiki yaliyojitokeza baada ya kutumia dawa ambazo zimefumua mfumo wa mtitiriko wa tishu za mwili.
“Kwa sasa naishi maisha mabaya… natakiwa kuwa mwangalifu saana maana nimejikuta nasumbuliwa na aleji ya mara kwa mara…nah ii ni kutokana na zile sindano nilizochomwa ili kuunda upya mwili wangu.”
Anasema kuwa anakumbuka kuwa na kiu ya kuwa na mwonekano kama ule wa mwanamuziki Janet Jackoson ama J-Lo, ambao mara zote huonekana nadhifu na wanawake wenye kuvutia machoni mwa watu kutokana na maumbile yao kuwa na mvuto wa ajabu.
Anakumbuka mwaka 2004 ndiyo ulibadilisha historia ya maisha yake pale alipokutana na dada mmoja, ambaye baada ya majadiliano ya muda mfupi alichukua uamuzi wa kuchomwa sindano hatimaye mwili wake upate madiliko makubwa kwa kufanana na wale kinadada aliowataja.
Apryl ambaye ni mkazi katika jiji la Los Angeles, Marekani anasema kuwa: “Nilipozungumza na yule dada na namna alivyonionyesha kuwa ni mtu mwenye kuelewa mambo mengi nilikubali wazo la kuchomwa sindano ya kubadilisha mwonekano wa mwili wangu.”
“Nilichomwa sindano mara mbili kisha nikatulia….kusema kweli uamuzi ule ulikuwa kama kujitakia kifo.”
Inasemekana kuwa dada aliyemchoma sindano hiyo alikuwa hana utalamu wowote wa utabibu mbali ya kutaka fedha kwa ajili ya kuendeshea maisha yake. Inaelezwa kwamba alilipwa kiasi cha pauni za Uingereza 650.
Madaktari walioendesha uchunguzi waligundua kuwa dawa iliyotumika kwa dada huyo ilikuwa na madhara makubwa kwa mwili wa binadamu, kwani ilitengenezwa maalumu kwa ajili ya kutumika katika viwanda.
Shauku yangu ya kutaka kuwa na mwonekano mpya na namna nilivyomwamini dada yule nikachukua uamuzi wa mara moja kuruhusu nichomwe sindano ile. Nilimwamini sana yule dada kwa vile alionekana kama mweledi na mtaalamu aliyebobea.”

source: Mwananchi news paper