Kwa ufupi
- Katika hukumu iliyosomwa leo jioni, mahakama 
imesisitiza kuwa kwa kulazimisha viongozi watoke vyama vya siasa, 
Tanzania inawanyima wananchi wake fursa huru ya kushiriki kwenye 
uongozi
 
 
Arusha. Mwanasiasa mkongwe 
nchini Christopher Mtikila ameshinda kesi aliyofungua Mahakama ya Haki 
za Binadamu ya Afrika (AfCHPR) mjini Arusha akidai Tanzania inakiuka 
demokrasia inapozuia wagombea binafsi.
Katika hukumu iliyosomwa leo jioni, mahakama 
imesisitiza kuwa kwa kulazimisha viongozi watoke vyama vya siasa, 
Tanzania inawanyima wananchi wake fursa huru ya kushiriki kwenye 
uongozi.
Mchungaji Mtikila, ambaye ana historia ndefu ya 
kukwaruzana na serikali ya Chama Cha Mapinduzi, alifungua shauri 
mahakama ya Afrika mwaka 2011 baada ya jitihada zake za kupindua 
mabadiliko ya kikatiba yaliyofuta ugombea binafsi kugonga mwamba kwenye 
mahakama za kitaifa.