Saturday 21 September 2013

Chadema Same kumng’oa mbunge

Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi, Dk David Mathayo David, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi akifafanua jambo Bungeni 
Na Daniel Mjema,Mwananchi

Posted  Septemba21  2013  saa 9:37 AM
Kwa ufupi
Operesheni hiyo iliyopewa jina la “Operesheni Mathayo Out” kwa kifupi OMO ilianza wiki iliyopita kwa kufanya mikutano ya hadhara jimboni humo na itaendelea tena wiki ijayo.


Same. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza operesheni maalumu ya kumng’oa ubunge, Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi, Dk David Mathayo David katika Uchanguzi Mkuu wa 2015.
Operesheni hiyo iliyopewa jina la “Operesheni Mathayo Out” kwa kifupi OMO ilianza wiki iliyopita kwa kufanya mikutano ya hadhara jimboni humo na itaendelea tena wiki ijayo.
Mmoja wa makamanda wa operesheni hiyo, Gervas Mgonja alisema jimbo hilo limekuwa chini ya himaya ya CCM tangu Uhuru lakini wananchi wake wapo kama wamefunga ndoa na tatizo la maji.
Dk Mathayo ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi alipoulizwa kuhusu operesheni hiyo ya kumng’oa alisema, Chadema ni chama kidogo na hakimnyi usingizi kwa madai uwezo wa kampeni unaishi

SOURCE: MWANANCHI