Monday 23 September 2013

Raisi wa Kenya Uhuru Kenyata amewaomba wakenya kuwa watulivu


Raisi wa Kenya uhuru kenyata amewaomba wakenya kuwa watulivu wakati Huu   ambapo vikosi vya usalama vinafanya jitihada kuhakikisha watu waliobaki kaitka jengo la WEST GATE wanaokolewa huku akisisitiza kuwa serikli yake itapambana na magaidi popote pale walipo.
Rais Kenyatta ametoa kauli hiyo  wakati akihutubia taifa jana  juu ya tukio la kuuwawa kwa watu wapatao 68 na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa,ambapo alitoa hotuba hiyo  mbele ya ya viongozi mbalimbali  wa kisiasa akiwemo aliekuwa waziri mkuu wan chi hiyo  raila odinga. Aidha rais uhuru kenyatta amesema vita hii  haihusu dini yoyote wala kabila lolote bali ni vita ya ugaidi.
Tukio hilo limetokea tangu jumamosi sept 21 ambapo mpaka sasa bado kuna watu wameshikiliwa na wavamizi hao ndani ya jengo hilo la WEST GATE MALL lakini serikali ya kenya imewahakikishia wananchi kuwa inafanya jitihada zote kuwaokoa watu walioko ndani ya jengo hilo.
 
Askari wa Kenya wakiwa katika harakati za uokoaji
Hali ilivyokuwa katika Jengo la WEST GATE MALL