Tuesday 29 October 2013

Dola inakandamiza vyombo vya habari, asema Kibanda


 “Wadau wote wa habari wanatakiwa kutambua kuwa uhuru wa habari wa kujieleza na kuhabarisha ni haki ya msingi ya kila Mtanzania ingawa mamlaka zikandamiza haki hiyo.” Absalom Kibanda 
Na Hakimu Mwafongo, Mwanananchi

Posted  Jumatatu,Oktoba28  2013  saa 11:1 AM


Dola na mamlaka nyingi za nchi, zinaendelea kukandamiza vyombo vya habari na kudidimiza haki ya watu kupata habari.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, baada ya kutembelea mnara wa kumbukumbu ya mauaji ya mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel ten mkoani Iringa, Daud Mwangosi.
Mnara huo umejengwa  katika Kijiji cha Nyololo wilayani Mufindi.
 Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari, alisema wanahabari mkoani Iringa wametembelea eneo hilo, ili kuonyesha mshikamano wao katika kuihabarisha jamii.
 Pia alisema wahariri ambao hawakupata fursa ya kufika eneo hilo wakati wa mauaji ya mwandishi huyo, wameweza kuipata kumkumbuka ya Mwangosi ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Iringa.
 Alisema jambo walilofanya linatoa ujumbe kwa mamlaka na vyombo vya dola kutambua haki ya uhuru wa habari na kujieleza.
 “Wadau wote wa habari wanatakiwa kutambua kuwa uhuru wa habari wa kujieleza na kuhabarisha ni haki ya msingi ya kila Mtanzania ingawa mamlaka zikandamiza haki hiyo,” alisema.
 Mjumbe wa jukwaa hilo, Theophil Makunga, alisema Mwangosi aliuawa akimtetea mwandishi mwenzake wa Gazeti la Nipashe, Godfrey Mushi aliyekuwa akipigwa na askari katika vurugu zilizotokea katika mikutano ya Chadema, kijijini  Nyololo.

SOURCE: MWANANCHI