Alisema thamani ya wanyama wote waliotoroshwa ilikuwa ni Sh170.5 milioni
 na kwamba twiga hao wanne kila mmoja alikuwa na thamani ya Dola 10,000 
za Marekani sawa Sh60 milioni za Tanzania. PICHA|MAKTABA 
            
    Na Waandishi Wetu,Mwananchi
Posted Alhamisi,Oktoba31 2013 saa 24:0 AM
Posted Alhamisi,Oktoba31 2013 saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Madai hayo yalitolewa jana na shahidi wa 13 katika 
kesi kuhusu utoroshaji wa wanyama hai kupitia Uwanja wa Ndege wa 
Kimataifa wa Kilimanjaro
Moshi na Dodoma. Mahakama ya 
Hakimu Mkazi mjini Moshi, imeelezwa kuwa marubani wa ndege ya kijeshi ya
 Qatar, walitumika katika kutorosha twiga wanne kwenda Uarabuni na 
kwamba washtakiwa walikuwa na hati za kusafiria zenye hadhi ya 
kidiplomasia.
Shahidi wa 13, Prisca Sabugo ambaye ni Ofisa 
Uhamiaji, aliiambia mahakama juzi kuwa hati hizo hazikugongwa mihuri 
wala kupewa viza.
Akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi 
Mfawidhi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Kobelo, shahidi huyo alidai kuwa 
ndege hiyo ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro 
(Kia) Novemba 24 mwaka 2011.
“Baada ya hiyo ndege ya jeshi kutua, alikuja 
wakala wao kutoka Kampuni ya Equity Aviation akaniletea Diplomatic 
Passport zao na akaniambia wamekuja kwa shughuli za utalii kwa siku 
tatu,” alisema.
Huku akiongozwa na mawakili wa Serikali, Evetha 
Mushi na Joseph Maugo, shahidi huyo alidai kuwa marubani na wafanyakazi 
wa ndege huwa hawapitii utaratibu wa kawaida wa kujaza fomu na kupewa 
viza. Alisema, tangu wageni hao waingie nchini kama watalii, hawakuwahi 
kuhojiwa na chombo chochote kuhusu kutogongwa mihuri kwenye hati zao.
Shahidi wa 12, Oscar Jullius ambaye ni Ofisa 
Wanyamapori, alidai kuwa vibali vilivyotumika kukamata wanyama hao 
vilikuwa vya kampuni mbili ambazo ni Ham Market na Luega Birds Traders.
Kwa mujibu wa shahidi huyo, vibali hivyo vilikuwa 
vya kumiliki nyara na si vya kukamata wanyamapori hai na kwamba yeye 
ndiye aliyeandika ripoti ya thamani ya wanyama hao.
Alisema thamani ya wanyama wote waliotoroshwa 
ilikuwa ni Sh170.5 milioni na kwamba twiga hao wanne kila mmoja alikuwa 
na thamani ya Dola 10,000 za Marekani sawa Sh60 milioni za Tanzania.
Alipoulizwa na mmoja wa mawakili wanaowatetea 
washtakiwa, Edmund Ngemela, kama vibali walivyokuwa navyo vilikuwa 
halali, alikiri kuwa vilikuwa halali na vilikuwa ni vya kumiliki nyara.
Kesi hiyo imepangwa kuendelea Novemba 29 mwaka huu.
Washtakiwa katika kesi hiyo ni pamoja na raia wa 
Pakistan, Kamran Ahmed, Hawa Mang’unyuka, Martin Kimath na Michael Mrutu
 ambao wote wako nje kwa dhamana.
Katika hatua nyingine, madiwani watatu wa 
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro akiwamo mwenyekiti wa halmashauri 
hiyo, wanashikiliwa na maofisa wa Kikosi cha Maalumu cha Kupambana na 
ujangili.
SOURCE : MWANANCHI
Huko Dodoma, watu sita wamekamatwa na polisi wilayani Kondoa 
baada ya kupatikana na vipande vinane vya meno ya ndovu yenye thamani ya
 Sh 25mil.
ioni.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma Suzan Kaganda,
 aliwambia waandishi wa habari jana kuwa, watuhumiwa hao walikamatwa 
katika operesheni maalum ya kupambana na ujangili.
SOURCE : MWANANCHI

