Thursday 31 October 2013

Walionaswa wakiuza mkono wa mtu wafikia wane


Na Frederick Katulanda, Mwananchi

Posted  Alhamisi,Oktoba31  2013  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
“Tumefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mwingine, kwa sasa tunafanya uchunguzi, siwezi kuthibitisha kama ni mtumishi wa Serikali au la,”


Mwanza. Jeshi la Polisi limemnasa mtu mwingine na kumuunganisha katika kesi ya kukutwa na kiganja cha mkono wa binadamu. Kukamatwa kwa mtu huyo, kunafanya watuhumiwa waliotiwa nguvuni mpaka sasa kufikia wanne.
Taarifa kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zilizothibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi, Joseph Konyo zimesema mtuhumiwa huyo anayedaiwa kuwa ni mtumishi wa Serikali Idara ya Afya, ndiye aliyefanikisha kupatikana kwa kiganja hicho.
“Tumefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mwingine, kwa sasa tunafanya uchunguzi, siwezi kuthibitisha kama ni mtumishi wa Serikali au la,” alisema Konyo.
Watuhumiwa wengine watatu walinaswa Novemba 28 mwaka huu eneo la Ziwani, Uwanja wa Ndege wa Mwanza wakiwa katika jitihada za kuuza mkono huo baada ya kuwekewa mtego na polisi.
Konyo alisema kazi ya kuwakamata watuhumiwa wengine kuhusiana na tukio hilo inaendelea.
“Kufanikiwa kumnasa mtuhumiwa huyu ni mafanikio makubwa kwa vile inaonekana ndiye anafahamu kila kitu kuhusu kiganja hicho kilipatikana wapi na kwa namna gani,” alisema Konyo.

SOURCE: MWANANCHI