Sunday 13 October 2013

Mtangazaji wa itv apigwa risasi, mama yake auwawa na mume wake kujiua!

Pichani ni mtangazaji wa kituo cha Television cha ITV Ufo Saro katika picha ya pamoja na Rais Jakaya Kikwete alipokutana na waandishi mbalimbali Ikulu Decemba 12, 2012 (Picha kutoka Maktaba)

Kuna taarifa kwamba mtangazaji wa kituo cha Television cha ITV (Ufo Saro) amepigwa risasi na kujeruhiwa vibaya huko maeneo ya Kibamba leo Alfajiri na mama yake mzazi kuuliwa. habari zaidi zinasema kwamba aliyefyatua Risasi hizo ni mchumba wa Mtangazaji huyo anayefanya kazi katika shirika moja la UN, ambaye baada ya tukio hilo naye alijipiga risasi na kujiua. 

Maisha Times Blog inaendelea kufuatilia tukio hili la kuhuzunisha na punde itakuletea habari hii kwa kina. Endelea kuwa nasi.

Source: Breaking News - Radio One