Saturday, 7 September 2013

Fast Jet sasa kusafirisha mizigo




Na Mwandishi wetu, Mwananchi

Posted  Septemba7  2013  saa 11:57 AM
Kwa ufupi
Ofisa Biashara Mkuu wa Fast Jet, Richard Bodin, alisema chini ya mkataba huo Watanzania wanaweza kusafirisha mizigo yao ndani ya nchi kwa kutumia kampuni hiyo.


Dar es Salaam. Kampuni ya Ndege ya Fast Jet, imeingia makubaliano na Kampuni ya kusafirisha mizigo ya Afrika ya BidAir, kusafirisha mizigo kwa kutumia ndege.
Ofisa Biashara Mkuu wa Fast Jet, Richard Bodin, alisema chini ya mkataba huo Watanzania wanaweza kusafirisha mizigo yao ndani ya nchi kwa kutumia kampuni hiyo.
Alisema awali wateja wa Fast Jet Tanzania, walikuwa hawana fursa ya kusafirisha mizigo mikubwa, lakini kwa sasa wanaweza kufanya hivyo lakini kwa kupitia Kampuni ya BidAir.

source: Mwananchi