Thursday 3 October 2013

Dr. Slaa Anaendelea Kutafuta Ufumbuzi Wa Tatizo La Kiuchumi. Makampuni yaahidi Maelfu ya Ajira!


Dr. Slaa Kwenye picha ya pamoja na wakuu wa mashirika makubwa yanayotengeneza mashine nzito za ujenzi na shuguli nyingine za viwanda. Wote wako tayari kufanya kazi Tanzania na kutengeneza maelufu ya ajira kwa watanzania kama CHADEMA watamn'goa adui UFISADI unaoendelezwa na CCM
Leo asubuhi Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mh. Wilbrod Slaa Washington DC kuelekea jimbo la North Carolina ambako amelakiwa na Rais wa Chuo cha Piedmond Community College yenye jumla ya campuses 16. Na jumla ya wanafunzi 85,000
Piedmont Community College ndio moja ya Community colleges bora zaidi Marekani, na imekuwa ikitayarisha wanafunzi mahiri kwenye eneo la engineering.
Lengo kubwa la kiongozi huyu maarufu nchini kukutana na Rais wa Chuo, ni kujifunza siri ya mafanikio ya chuo hicho, kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi wa kitanzania kufanya vizuri zaidi kwa lengo kubwa la kutayarisha rasilimali watu. Dr. Slaa pamoja na chama cha Chadema, wanaamini kwamba, ili kuliokoa taifa, lazima elimu ipewe nafasi ya kwanza
Kadhalika, Dr. Slaa na Rais was chuo kikuu cha Pedmont walikubaliana kuanzisha program maalum itakayowawezesha vijana wa kitanzania na wakimarekani kuanzisha urafiki utakaoziwezesha chuo hicho maarufu kufanya kazi kwa ukaribu na vyuo vya kitanzania. Vyuo vya kitanzania vitanufaika zaidi hasa kutokana na technologia ya kipekee ambayo hipo chuoni hapo
Dr. Slaa akipokelewa na viongozi wa Chuo Kikuu cha Central piedmont
Mitambo maalum inayotumika katika mafundisho ya viwandani. Hii ni kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi wanaochukua kozi ya kuendesha mashine viwandani.

Dr. Slaa akitizama kwa umakin jinsi mitambo hii ya kisasa inavyofanya kazi kati hiki chuo


Dr. Slaa na Mkewe wakionyeshwa mtambo mdogo wa aina yake, ambayo inaweza kusafisha maji machafu kwa ajili ya binadamu. Huu mtambo ni wa aina yake na gharama nafuu sana na inaweza kutengeneza(safisha) lita 500 kwa siku huku ikitumia mionzi ya jua yaani solar. CHADEMA itanunua hii mitambo na kuyasambaza vijijini kupunguza tatizo la maji safi huku ikitafuta suluhisho la kudumu

Dr. slaa pamoja na viongzi wa juu wa Charlotte Chamber of commerce kwenye picha ya pamoja baada ya kufanya maongezi ya ushirikiano wa kibiashara
Dr. Slaa akiwa kwenye maongezi na Rais wa Chuo cha Piedmont

Dr. Slaa akionyeshwa jinsi mitambo ya kisasa inayotumika katika mafunzo inavyofanya kazi. Hii karakana ndiyo inayotumika kuwatayarisha vijana kuwa wabunifu na kuweza kijiajiri

Mitambo maalum inayotumika katika mafundisho ya viwandani. Hii ni kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi wanaochukua kozi ya kuendesha mashine viwandani.

Baada ya miaka 52 ya ufisadi na kuuzwa kwa rasilimali za nchi, elimu duni, umasikini wa kupindukia, huku taifa likiendelea kuwa omba omba Dr. Slaa pamoja na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo imeamua kutafuta njia mbadala ya kuleta ukombozi karibu na wananchi. Chadema imeanza kutafuta mbinu za kumkomboa mtanzania kutoka kwenye ufukara. Lengo la Chadema ni kutengeneza mamilioni ya ajira ambazo makampuni mengi yako tayari kuyazalisha kama Chadema itatengeneza mazingira mazuri ya wao kuwekeza.

Dr. Slaa amemaliza ziara ya siku moja carolina na kuondoka kuelekea Atlanta georgia ambako atakutana na viongozi wa shirika la Coca-Cola, AT&T pamoja UPS
SOURCE: CHADEMA DIASPORA BLOG