Friday 13 September 2013

"Rejesheni matumaini’

Posted  Alhamisi,Septemba12  2013  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Waziri Malima aliyasema hayo mkoani Morogoro wakati akifungua mafunzo hayo yaliyoshirikisha mikoa ya Mbeya, Iringa.


Morogoro. Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adamu Malima amewataka wahitimu wa mafunzo ya ukaguzi na udhibiti wa mbolea, awamu ya nne kutumia mafunzo waliyoyapata ili kukidhi matarajio ya wakulima walio kata tamaa kwa muda mrefu kutokana na uwapo wa mbolea zisizo na viwango vya ubora.
Waziri Malima aliyasema hayo mkoani Morogoro wakati akifungua mafunzo hayo yaliyoshirikisha mikoa ya Mbeya, Iringa, Tabora, Siminyu, Morogoro, Mwanza na Shinyanga na kudai kuwa yatasaidia kutatua tatizo la uchakachuaji mbolea unaofanywa na watu wasio waaminifu na kuwataka wasimamie kwa weledi sheria ya mbolea namba 9 ya mwaka 2009.
Naibu waziri huyo wa kilimo, aliwataka wakaguzi na wadhibiti wa ubora wa mbolea hao waliopata mafunzo hayo kurejesha imani na matarajio ya wakulima.
SOURCE: MWANANCHI