Tuesday 1 October 2013

Tanzania, Zambia zajipanga kuboresha usafirishaji

Tanzania na Zambia zimeamua kuchukua hatua za ziada kujaribu kuboresha usafiri kati ya nchi hizo mbili, ambazo tayari zina ushirikiano wa muda mrefu kupitia shirika la reli la Tazara. PICHA | FAILI 
Na Lauden Mwambona

Posted  Jumanne,Oktoba1  2013  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Naibu Kamishna Mkuu wa Mamalaka ya Kodi Tanzania (TRA), Rished Bade, ambaye kwa jana alikuwa mkuu wa msafara, alisema ujumbe wake utakuwa na mazungumza na wenzao wa Zambia kwa nia ya kuboresha utendaji na kuimarisha uhusiano.

Mbeya. Tanzania na Zambia zimeanza mazungumzo maalumu ya kutafuta mbinu za kuboresha utendaji kazi wa kusafirisha mizigo kwenye mpaka wa nchi hizo, uliopo Tunduma.
Tayari, ujumbe wa zaidi ya watu 20 kutoka Wizara za Uchukuzi, Fedha, Mambo ya Ndani na wadau wa usafirishaji waliwasili jijini Mbeya tangu juzi, jana walikwenda Tunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia kujionea utendaji ulivyo kwa upande wa Tanzania.
Naibu Kamishna Mkuu wa Mamalaka ya Kodi Tanzania (TRA), Rished Bade, ambaye kwa jana alikuwa mkuu wa msafara, alisema ujumbe wake utakuwa na mazungumza na wenzao wa Zambia kwa nia ya kuboresha utendaji na kuimarisha uhusiano.
Bade alisema baada ya ujumbe,  kitafuata kikao cha makatibu wakuu wa wizara zote zinazohusika za Tanzania na zile za Zambia kitakachofanyika Oktoba 3.
 “Pamoja na mengineyo, lengo kubwa ni kuandaa taratibu za kuanza ujenzi wa kituo kimoja  cha mpakani kwa magari yote ya Zambia  na Tanzania ( One Stop Boarder Post), ili kuondokana na usumbufu wa sasa,” alisema.
Alisema tayari ujumbe wa Zambia walikuwa wakijiandaa kwenye Mji wa Nakonde  nchini Zambia, kabla ya kukutana kuanzia kesho.

SOURCE: MWANANCHI