Thursday 5 September 2013

RC amsaidia mwandishi


Na Mwandishi Wetu  (email the author)

Posted  Jumatano,Septemba4  2013  saa 20:20 PM
Kwa ufupi
Huyu mwandishi alifika ofisini akanieleza shida yake na nimempa haya mabati kama mwananchi wa kawaida wa Kisarawe na mkazi wa mkoa wangu huu, si kama mwanahabari.


Kibaha. Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza amemsaidia mwandishi wa habari wa Kampuni ya The Guardian, Amri Lugungulo mabati 100 yenye thamani ya Sh1.5 milioni kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa nyumba na kuweza kuondokana na adha ya nyumba za kupanga.
Mwandishi huyo alikabidhiwa rasmi mabati hayo jana katika ofisi ya mkuu huyo wa mkoa na kushuhudiwa na wanahabari wa vyombo mbalimbali nchini. Mahiza pia amempa fedha taslimu Sh100,000 kwa ajili ya kusafirishia mabati hayo kwenda wilayani Kisarawe anakojenga nyumba yake mwandishi huyo.
“Huyu mwandishi alifika ofisini akanieleza shida yake na nimempa haya mabati kama mwananchi wa kawaida wa Kisarawe na mkazi wa mkoa wangu huu, si kama mwanahabari, maana mimi kama mkuu wa mkoa wapo watu ambao huja kunieleza shida zao na kama nikiona upo umuhimu zaidi ya kumsaidia nasaidia kulingana na hitaji la mtu baada ya kuthibitisha ukweli wa shida yake,”alisema Mahiza.
Lugungulo ameshukuru kwa msaada huo, alisema umemfikia kwa wakati kutokana na uhitaji aliokuwa nao ili aweze kuezeka nyumba yake anayoijenga huko Tabata na aondokane na kero za nyumba za kupanga anayoishi kwa zaidi ya miaka kadhaa sasa huko Buguruni, Dar Salaam. Lugungulo amefanya kazi katika vyombo vya habari ikiwamo Daily news,Uhuru na Mzalendo,Nipashe na sasa The Guardian

Source: Mwananchi