Kwa ufupi
- Zaidi ya watu 3000 waliuawa
 
Taifa la Marekani jana limetimiza miaka 12 tangu
 Septemba 11, mwaka 2001, yalipotokea mashambulizi ya kigaidi  kwenye 
miji ya  New York  na Washington DC .
Mashambulizi hayo yalisababisha watu  takribani  
3,000  kupoteza maisha na kuliweka taifa  hilo kwenye majonzi mazito ya 
kupotelewa na wapendwa  wao.
Kutokea kwa mashambulizi hayo kuliacha mshangao 
mkubwa kwa  Taifa la Marekani ambalo lilidhaniwa kuwa lipo imara 
kiusalama na  lisingeweza kushambuliwa  kwenye  ardhi yake kama 
ilivyotokea.
Hali ilivyokuwa
Tukio hilo lilipotokea  Jiji la New York  na 
Washington DC, anga lilionekana kuchafuka kwa moshi wakati ndege mbili 
za abiria zilizotekwa zilipogonga katika minara ya majengo ya biashara 
(World Trade Center ). Ndege  nyingine ziligonga  kwenye  makao makuu ya
 Wizara ya Ulinzi ya Marekani  Pentagon. Tukio hilo kwa ujumla lilizua 
mshangao mkubwa duniani kutokana na imani ya wengi kwamba Marekani ni 
taifa kubwa na lenye ulinzi imara.
Ndege nyingine watekaji walidhibitiwa
Katika hatua nyingine ndege ya nne iliyotekwa 
ilianguka karibu na mji mdogo wa Shanksville, Pennsylvania, baada ya 
abiria kupambana na watekaji na kuchukua udhibiti wa ndege hiyo.
Taifa hilo tajiri duniani baadaye lilibadili idara
 zake za ulinzi wa ndani na kubadili sheria ili kuzuia uwezekano wa 
mashambulizi mengine kama hayo kutokea.
Al Qaeda yahusishwa.
Tukio hilo kubwa kutokea duniani liliwahusisha wafuasi wa mtandao wa al Qaeda .
Serikali ya wakati huo ilikuwa inaongozwa na Rais 
mstaafu  George Bush, baada ya kutokea kwa tukio hilo  mtandao wa al 
Qaeda ulihusishwa na mashambulio hayo moja kwa moja.
Kumtafuta  Osama
Baada ya Serikali ya Marekani kuihusisha al Qaeda, iliamua 
kuivamia nchi ya Afghanistan na Iraq  na kuzishambulia nchi hizo kwa 
lengo la kumsaka kiongozi wa Al Qaeda  Osama Bin Laden ambaye ndiye 
aliyehusishwa kupanga njama za kuishambulia Marekani.
Hata hivyo tokea wakati huo ilikuwa ikijulikana 
kuwa Al Qaeda ni kundi lililoundwa na Shirika la Ujasusi la Marekani CIA
 muongo mmoja kabla ya hapo wakati wa vita dhidi ya majeshi ya Urusi ya 
zamani nchini Afghanistan.
Viongozi wakuu wa kundi hilo hususan ukoo wa Bin 
Laden ulikuwa na uhusiano wa karibu wa kibiashara na baadhi ya wanasiasa
 nchini Marekani wakiwemo wa ukoo wa Bush.
Jambo hilo lilisababisha baada ya kutokea kwa 
tukio hilo Septemba 11.Mashambulizi ya maneno dhidi ya Osama Bin Laden 
yaliyofuatiwa na uvamizi wa majeshi ya Marekani nchini Afghanistan.
Tangu  Marekani ilipoivamia Afghanistan,  wasomi 
wa Marekani walieleza bayana kuwa sera za uingiliaji wa kijeshi za 
Serikali zilizopita, ndizo zilizosababisha kutokea matukio ya umwagaji 
damu ya Septemba 11.
Kwa mtazamo wa wasomi na wanafikra hao, kama  
Serikali zilizopita nchini Marekani zisingeunga mkono ukiukaji wa wazi 
wa misingi ya demokrasia na haki za binadamu katika pembe mbalimbali 
duniani na kusababisha maafa kadhaa wakati wa vita ya Ghuba ya Uajemi ya
 mwaka 1991, huenda magaidi wasingehangaika na Marekani.
Obama anakumbuka
Wakati Wamarekani wanakumbuka na kuadhimisha siku 
hiyo, Rais wa Marekani Barack Obama ametembelea  maeneo yote ambayo 
mashambulizi yalitokea.
Katika hotuba yake ya kila wiki alisifu watu 
waliofanya kazi za uokoaji ambapo  walijaribu kuokoa maisha ya wahanga 
wakati wa mashambulizi hayo.
Mapema mwaka huu, vikosi maalum vya Marekani 
vilifanikiwa kumwua kiongozi wa Al-Qaida Osama bin Laden huko Pakistan 
na kutimiza ahadi aliyoitoa rais wa zamani wa Marekani George W. Bush.
Hakuna hotuba
Kwa mara ya kwanza kwenye maadhimisho ya tukio hilo hakukuwepo na hotuba yoyote wakati wa sherehe hizo kutoka
Familia za zaidi ya watu waliouawa ziliruhusiwa  kufika katika 
eneo la tukio la mashambulizi hayo maarufu kama Ground Zero mjini New 
York,.
Awali idara ya afya nchini Marekani ilitangaza 
kuwa manusura wa mashambulio hayo na wale waliowasaidia watapewa 
uchunguzi na matibabu ya takriban aina hamsini za saratani bila malipo, 
kwa sababu walivuta hewa iliyokuwa na sumu baada ya mashambulio hayo.
Makala hii imeandikwa na, Aidan Mhando kwa msaada wa Mashirika mbalimbali ya habari
SOURCE: MWANANCHI
kwa wanasiasa.SOURCE: MWANANCHI