Thursday 12 September 2013

Kigogo wa Ardhi apatikana na kesi ya kujibu


Na Tausi Ally

Posted  Jumatano,Septemba11  2013  saa 22:4 PM
Kwa ufupi
Washtakiwa hao wataanza kujitetea kuanzia Oktoba 16,17,18,24 na 25, mwaka huu na kudai kuwa watajitetea kwa njia ya kiapo na kwamba watakuwa na mashahidi 13.


Dar es Salaam.Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema kuwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Simon Lazaro na wenzake wawili wana kesi ya kujibu kuhusiana na matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa Sh100 milioni.
Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana alisema jana baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi tisa wa upande wa mashtaka pamoja na vielelezo 15 walivyoviwasilisha mahakamani hapo, amewaona washtakiwa wote wana kesi ya kujibu hivyo wanatakiwa kuanza kujitetea.
Washtakiwa hao wataanza kujitetea kuanzia Oktoba 16,17,18,24 na 25, mwaka huu na kudai kuwa watajitetea kwa njia ya kiapo na kwamba watakuwa na mashahidi 13.
Mbali na Lazaro, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi, Gerald Mango na Kaimu Mhasibu Mkuu wa tume hiyo, Charles Kijumbe. Kesi hiyo inasomwa huku Lazaro akiwa ni Mkurugenzi kamili katika idara hiyo.
SOURCE: MWANANCHI