Thursday 12 September 2013

Wanusurika kufa kwa pombe- Tanzania


Na Zainab Maeda

Posted  Alhamisi,Septemba12  2013  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Alisema baada ya kazi hiyo, watu hao walianza kunywa pombe ya kienyeji na ilipofika jioni watu 19 walipatwa na ugonjwa wa tumbo. Kamanda huyo alisema baadaye watu hao walipelekwa katika Zahanati ya kijiji hicho kwa matibabu.


Iringa. Zaidi ya watu 19 katika Kijiji cha Imega, katika Wilaya ya Kilolo, wamenusurika kufa baada ya kunywa pombe ya kienyeji inayodhaniwa kuwa na sumu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi alisema tukio hilo lilitokea juzi wakati watu hao walipokwenda kuhudhuria sherehe iliyoandaliwa na mzee mmoja. Kwa mujibu wa kamanda huyo, sherehe hizo zilikuwa ni za kumuaga binti yake aliyekuwa akiolewa.
Alisema baada ya kazi hiyo, watu hao walianza kunywa pombe ya kienyeji na ilipofika jioni watu 19 walipatwa na ugonjwa wa tumbo. Kamanda huyo alisema baadaye watu hao walipelekwa katika Zahanati ya kijiji hicho kwa matibabu.
Alisema wakati wakiendelea kupata matibabu ,mmoja wa watu hao, alizidiwa na kukimbizwa katika Hosptali ya Itunda kwa matibabu zaidi. Alisema uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa huenda pombe walioitumia ilikuwa na sumu.
“Pombe hiyo inatokana na mahindi na inasemakana mahindi hayo yalikuwa na dawa. Tunafanya uchunguzi,” alisema Mungi.
SOURCE: MWANANCHI