Saturday 14 September 2013

KILIMO: Zabibu zakosa soko Tz




Na Rachel Chibwete
Kwa ufupi
Kato alisema, wakulima wengi wa zabibu mkoani Dodoma, wameitikia wito wa kulima zao la zabibu lakini tatizo ni kukosa soko.


Dodoma. Uzalishaji wa zabibu sasa umekuwa mkubwa kuliko uwezo wa viwanda vinavyotengeneza mvinyo nchini,jambo linalosababisha wakulima kukosa soko la zao hilo.
Hayo yalisemwa na Meneja wa Kiwanda cha Kutengeneza Mvinyo cha Alko Vintages, Archard Kato alipokuwa akizungumza na gazeti hili ofisini kwake juzi.
Kato alisema, wakulima wengi wa zabibu mkoani Dodoma, wameitikia wito wa kulima zao la zabibu lakini tatizo ni kukosa soko.
Alisema hiyo inasababishwa na viwanda kuwa na uwezo mdogo wa kuzalisha mvinyo na nafasi ya kutunzia bidhaa zinazozalishwa.
“Inauma kuona wakulima wanakosa soko la mazao lakini hata sisi wadau, hatuna cha kufanya kwa sababu uwezo wetu wa kuzalisha ni mdogo kutokana na mashine tulizonazo,” alisema kato.
SOURCE: MWANANCHI