Saturday 21 September 2013

Nani kuvaa taji la Miss Tanzania leo?


Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred (wa pili kutoka kulia) akiwa na washiriki wa walioingia tano bora baada ya kunyakua taji hilo jijini Dar es Salaam. Miss Tanzania hakuvishwa taji kwa sababu waandaji walilisahau. Picha na Salhim Shao 
Na Herieth Makwetta, Mwananchi

Posted  Septemba21  2013  saa 10:17 AM
Kwa ufupi
Mshindi wa taji hilo mwaka huu atajinyakulia gari jipya na kitita cha fedha Ssh 8milioni kutoka kwa wadhamini wakuu wa mashindano hayo, Kampuni ya Bia ya Tanzania (TBL).


Dar es Salaam.: Mrithi wa Redds Miss Tanzania 2013, Brigiter Alfred atapatikana leo wakati warembo 30 watakapopanda jukwaani kwenye Uukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Mshindi wa taji hilo mwaka huu atajinyakulia gari jipya na kitita cha fedha Ssh 8milioni kutoka kwa wadhamini wakuu wa mashindano hayo, Kampuni ya Bia ya Tanzania (TBL).
Akizungumza jana Mkurugenzi wa Lino Agency ambao ndiyo waandaaji wa mashindano hayo, Hasheem Lundenga alisema taji la malkia mpya wa urembo Tanzania limeshaandaliwa na mshindi wa pili mwaka jana ndiye atakayemvisha mshindi.
“Redds Miss Tanzania 2012 namba mbili, Eugene Fabian ndiye atakayemvisha taji malkia mpya baada ya Miss Tanzania 2012 Brigiter Alfred anayemaliza muda wake kuwaepo Indonesia akijiandaa kuwania taji la Miss World mwaka huu hapo Septemba 28,” alisema.
Kwa hivi sasa, taji la Redd’s Miss Tanzania linashikiliwa na Miss Sinza, Brigiter Alfred, aliyelitwaa taji hilo mwaka jana na kukabidhiwa gari aina ya Noah na kitita cha Ssh milioni nane.
Mshindi wa taji la mwaka huu atakuwa wa 21 katika historia ya mashindano ya urembo nchini na ataiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia ya mwakani.
Meneja wa Redds Original, Victoria Kimaro alisema kuwa siri kubwa ya kuingiza fedha katika mashindano hayo ni kuchangia maendeleo ya sanaa nchini, kuwawezesha wasichana wadogo, kuvumbua vipaji mbalimbali vya kujitangaza kibiashara.
Mashindano hayo yamepangwa kuanza saa 2 usiku na yatapambwa na burudani za kila aina kutoka kwa wasanii maarufu wa ndani na nje. Wasanii hao ni Judith Wambura “ Lady Jaydee” na msanii wa kizazi kipya kutoka Uganda, Mike Ross.
Mshindi wa pili atapata sh 6.2milioni , wa tatu sh 4milioni, wa nne sh3 milioni, wa tano sh 2milioni, huku mshindi wa sita hadi 15 watapata sh 1.2milioni kila mmoja na waliobaki watajipoza kwa sh 700,000 kila mmoja.

SOURCE: MWANANCHI