Friday 6 September 2013

RC amtimua mkurugenzi katika kikao



Na Mwandishi wetu

Posted  Alhamisi,Septemba5  2013  saa 21:28 PM
Kwa ufupi
Ni kweli tumefukuzwa kwenye kikao lakini tunaomba ufumbuzi wa mgogoro wetu upatikiane kwa sababu haileti taswira nzuri kwa viongozi kufukuzana kwenye vikao.


Arusha, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo juzi aliwafukuza, Mkurugenzi na wakuu wote wa Idara za Halmashauri wa Jiji la Arusha, katika kikao cha kujadili mfumo wa matokeo makubwa sasa.
Jana walitarajiwa kujadiliwa katika kikao cha kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha.
Kikao hicho, kilifanyika juzi katika ukumbi namba 40 katika jengo la ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Arusha na kuwashirikisha wakuu wa wilaya zote za mkoa huo, wakurugenzi na wakuu wa idara za halmashauri.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho na ambazo zilithibitisha na baadhi ya wakuu wa idara, zilisema mkuu wa mkoa aliwafukuza kwa tuhuma za kukataa kutekeleza maagizo yake.
“Ni kweli tumefukuzwa kwenye kikao lakini tunaomba ufumbuzi wa mgogoro wetu upatikiane kwa sababu haileti taswira nzuri kwa viongozi kufukuzana kwenye vikao,”alisema mkuu mmoja wa idara ya Jiji la Arusha.
Maagizo, ambayo yamemwingiza katika mgogoro mkurugenzi wa jiji hilo ni kukataa, kuipa Kampuni ya Skytel, zabuni ya kuendesha mradi wa taa za barabarani.
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni, mkurugenzi huyo Sipora Liana, alisema anataka taratibu za sheria ya manunuzi ya umma zifuatwe .

source: Mwananchi