Thursday 12 September 2013

Wanaharakati wapatao 18 watembea kwa miguu kutoka jijini Arusha hadi Dar es salaam kupinga uwindaji haramu wa tembo.


  
Wanaharakati  wapatao 18  wametembea kwa miguu  kutoka jijini  Arusha hadi Dar  es salaam  wakiitaka  serikali kuchukua hatua za dhati  dhidi ya   uwindaji haramu  wa  tembo.
Wakizungumza  na  waandishi  wa habari   baadhi  ya  wanaharakati  hao wamesema  vitendo  vya  kuuwa  kwa  tembo vinawasikitisha   na hivyo  wanataka kila mtu  pamoja  na serikali wachukue  hatua kudhibiti hali hiyo
Naye  mwenekiti wa kamati ya bunge ardhi  mazingira na maliasili   Mh James Lembeli  ameonyesha kukerwa na vitendo  vya baadhia ya magari ya serikali  kukamatwa yakiwa yamebeba   pembe za ndovu na huku wahuska wakiwa hawachukuliwi  hatua zozote
Akipokea na kuhitimisha  matembezi hayo naibu waziri wa  maliasili na utalii Mh  Lazaro Nyalandu amesema tatizo  la ujangili ni kubwa kuliko watu wanavyodhani  na hivyo ameaahidi   kuwa serikali  itawasaka wale wote wanaohusika na kuwachukulia hatua.
source: ITV-DAIMA