Monday 2 September 2013

‘Wajanja wanatorosha Dola 2 bilioni



Na Mussa Juma, Mwananchi  (email the author)

Posted  Agosti31  2013  saa 23:14 PM
Kwa ufupi
Zitto alitoa taarifa hiyo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha.


Arusha. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali,(PAC) Zitto Kabwe amesema kiasi cha Dola 2 bilioni za Marekani, zinapotea serikalini kila mwaka kwa kutoroshwa nje ya nchi au katika ukwepaji wa kodi .
Zitto alitoa taarifa hiyo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha.
Zitto, alisema hata hivyo tatizo hilo, si tu kwa Tanzania pekee yake na kwamba taarifa za kimataifa zinaeleza kuwa kwa bara la Afrika , kiasi cha Dola 700 bilioni zanatoroshwa nje ya bara kila mwaka.
Alisema fedha hizo ni zaidi ya misaada yote inayotolewa kwa nchi za Afrika.