Saturday 2 November 2013

Mwanamke abakwa, alawitiwa hadi kufa Moshi

2nd November 2013
Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz
Watu wasiojulikana, walimvamia mwanamke mmoja wa kijiji cha Mrimbo Uuwo, Mwika mkoani  Kilimanjaro nyumbani kwake wakambaka na kumlawiti hadi kupoteza maisha.

Akizungunza na NIPASHE, Afisa mtendaji wa kijiji hicho, Elizabert Mkonyi, alisema mama huyo alivamiwa juzi saa 3 usiku na kufanyiwa unyama huo na baadaye kufungwa mikono na miguu.

Alisema, mama huyo alikutwa ndani kwake akiwa amefanyiwa unyama huo, huku chakula chake cha jioni kikiwa mezani na watu huo kutokomea na magodoro mawili.
“Tulitoa taarifa kwa jeshi la polisi na mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya Kilema,” alisema Mkonyi.

Hata hivyo NIPASHE ilipomuuliza Mkuu wa Jeshi la polisi kuhusu kutokea kwa tukio hilo, hakupatikana na alipotafutwa kwa njia ya ujumbe mfupi kupitia simu yake ya kiganjani alijibu: "Nina dharura nitakutafuta."
 
CHANZO: NIPASHE