Sunday 10 November 2013

UKISTAAJABU YA MWIGAMBA UTAONA YA ZITTO KAZI NDIO KWANZA IMEANZA

 Theo Mutahaba amjibu Zitto Ndg. Zitto Nasikitishwa sana na hizi tabia zako za ajabu ajabu. Mimi nafanya kazi katika moja ya taasisi za ki usalama na nimeshirkia mara kadhaa kukupa fedha. Nyendo zako hata na sisi tunazijua na nimeshangazwa na utoto wako wa kuandika waraka ambao umetoa vitisho ambayo inadaiwa kutoka kwa Andrea Codes. Ndugu napenda kukuonya kwamba umefanya mengi ambayo hata wana Chadema hawajui. ·


 Swala la Bomu Arusha ulishiriki na lengo ilikuwa ni kumuua mwenyekiti wa Chadema pamoja na Ndg. Lema. Hii kitu ulipanga, wewe, mwigulu na vyombo vya usalama ·Zitto, rais Kikwete alipoenda Sudan ya Kusini uliambatana naye. Unakumbuka sababu ya wewe kuitwa? Nikukumbushie kwamba ilikuwa zawadi kwako ya kuihujumu chadema. CCM hawakupendi, bali wanapenda hujuma zako ndio maana walikudanganya kwamba watakusaidia kupata uenyekiti CDM ikiwepo kumuua Mbowe na kumdhoofisha Dr. Slaa ·

 Ndg. Zitto unadanganya umma kwamba unafuatilia fedha Uswisi wakati hii ni njama ambayo imesukwa na TISS kisha ukakabidhiwa ili CHADEMA isiibane sana serikali. · Tueleze ni majina gani uliyoyapata. Na kama umeyapata, tunaomba kujua jina lako ni namba ngapi, kwa sababu na wewe una fedha nje ya nchi na ushahuidi tunao · Umekuwa ukijenga mtandao wa kuwania uenyekiti na fedha ulizopewa na TISS pamoja na CCM ili kumn’goa Bw. Mbowe kwenye uenyekiti wa CHADEMA ili 2015 CCM ishinde. · Zitto, una ghorofa Dodoma karibu na St. Gasper Hotel. Fedha za kujenga lile jengo zimetoka wapi? · Zitto, Barrick gold walikujenga shule pale jimboni kwako. Baada ya lile shule kujengwa na pia kupewa kitita cha fedha ulinyamaza kabisa · 

Ndg. Zitto, wakuu wengi wa mashirika ya umma wameleta malalamiko TISS kuhusu unavyochukua fedha kwao. Hilo unalijua kama ni ufisadi? Ndg. Zitto, wewe ni kijana mdogo. Hizi tamaa zako za kifisadi zitaipeleka nchi pabaya. Tunakuangalia na kelele zako hasa fedha za uswisi. Usichezee na akili za watanzania. Wewe ni fisadi namba moja. Umeficha fedha nje, ama nikukumbushe kwamba, majuzi ulipokuwa nje ya nchi ulitoa fedha kwenye benki Fulani. Ile account umefunguliwa na nani? Badilika kijana. Kisiasa umeshajimaliza. Pengine nikukumbushie kwamba mawasiliano yako na Jack Nzoka, Mwigulu, Ridhiwani za kisaliti ndio chanzo cha kuanguka kwako. Ila hacha kuwadanganya watanzania na kiini macho cha Uswisi. Umeshajua mengi sana , usishangae kijana ukija kutoweka ghafla. 

TISS hawachezi na mtu. Na ni wao au CCM ndio watakao kumaliza sio CHADEMA. Ule waraka unaosambaa ni mali ya TISS na imeratibiwa na CCM ambao ndio ndugu zako wakubwa Andrea, take care of your son. Get out of these Zitto corrupt acts. you know quite well that we wired you money and we have the evidence. 

Why would you waste your effort making noises? do you know the German government is investigating this matter? why would you fall for Zitto childish internet games of writing emails to the Chadema leaders. So for your information, the document came from CCM and Tanzania Intelligence Services Nakutakia kila la kheri kwenye kuhujumu Chadema.