Sunday 6 October 2013

Mgomo wa madereva wa malori waingia siku ya pili Mizani Kibaha


 Idadi kubwa ya malori mizigo yanayokwenda mikoani na nje ya nchi yamekwama  katika mizani ya Kibaha mkoani Pwani kwa muda kutokana na kubainika kuwa na ongezeko kubwa la uzito wa mizigo lililo sababisha kutozwa kiwango kikubwa cha fedha kuliko viwango vilivyokuwa vikitozwa awali.

Wakizungumza na waandishi wa habari, madereva wa malori hayo wameilalamikia serikali kuweka utaraibu mpya wa upimaji unaoonyesha kuwepo kwa uzito mkubwa na tozo  bila ya kutoa elimu kwa wamiliki na madereva wa malori hali inayosababisha idadi kubwa ya malori kubainika kuwa na uzito mkubwa tofauti vipimo vya siku zilizopita.

Aidha Itv imeshuhudia malori yaliokuwa yamebeba gesi,mingine mafuta ya petroli na mafuta mazito yakiwa pamoja na malori ya mizigo ndani ya eneo la mizani hiyo hali ambayo ni hatari,ambapo wakizungumza na waandishi wa habari baadhi ya madereva wamesema kwa mujibu wa taratibu magari hayo yanatakiwa kutembea si zaidi ya masaa 12 na kusisitiza  kusimama kwa muda mrefu katika mizani hiyo kumesababisha kushindwa kufuata taratibu za usafirishaji..

SOURCE. ITV-DAIMA