Monday 4 November 2013

M23 yawataka wafuasi kusitisha mapigano

 4 Novemba, 2013 - Saa 05:22 GMT
Wanajeshi wa serikali ya DRC katika vita dhidi ya M23
Wanajeshi wa serikali katika Jmauhuri ya kidemokrasi ya Congo, wanashambulia ngome ya mwisho ya waasi wa M23 katika maeneo ya milimani ,msituni Mashariki mwa nchi.
Mamia ya wakimbizi wanatoroka vita karibu na mpaka wa Mashariki mwa Congo na kuingia nchini Uganda.
Viongozi wa kundi hilo la M23 walitoa wito kwa wapiganaji wao kusitisha vita na kuruhusu mazungumzo ya amani na serikali.
Kiongozi wa wapiganaji hao Mashariki mwa nchi ametangaza kuwa watasitisha mapigano katika vita vyao na jeshi la serikali.

Bertrand Bisimwa alisema kwenye taarifa kwamba anawasihi wapiganaji wote haraka waache uhasama na wanajeshi, ili kuwezesha mazungumzo ya amani kuendelea.

Wanajeshi wa serikali, wakisaidiwa na kikosi cha kuweka amani cha Umoja wa Mataifa, hivi karibuni wamewasukuma nyuma wapiganaji na kuwatoa katika ngome zao nchini.
Mazungumzo ya amani yanafanywa mjini Kampala, Uganda.

SOURCE: BBC SWAHILI