Tuesday 1 October 2013

Chadema, CUF, NCCR zalia na Serikali

NCCR, CHADEMA WALIA NA SERIKALI Kufuatia kikao cha zaidi ya saa mbili kati ya John Mnyika wa Chadema (pichani), Abdul Kambaya (CUF) na Faustine Sungura (NCCR-Mageuzi), vyama hivyo vinasema serikali haikufuata taratibu kuifungia Mwananchi na Mtanzania. PICHA  FAILI  
Na Fidelis Butahe,

Posted  Jumanne,Oktoba1  2013  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Chadema leo, Mkuu wa Oganaizesheni wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura alisema haiwezekani kwa Serikali kuwa mlalamikaji, mtetezi na jaji.

Dar es Salaam. Umoja wa vyama vitatu vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi vimesema Serikali haikufuata taratibu kufungia kuchapishwa kwa Magazeti ya Mwananchi na Mtanzania.
Viongozi wa kamati ya pamoja ya vyama hivyo, wamesema kuwa Serikali haikutenda haki kwa kuyafungia magazeti hayo badala yake, ilitakiwa kuwasilisha malalamiko yake Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Chadema leo, Mkuu wa Oganaizesheni wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura alisema haiwezekani kwa Serikali kuwa mlalamikaji, mtetezi na jaji.
Sungura alisema alikutana kwa saa mbili na viongozi wa vyama hivyo; John Mnyika (Chadema) na Abdul Kambaya (CUF) kujadili suala hilo.
Alisema watu wangependa kujua mtu aliyelalamikia habari zilizoandikwa na magazeti hayo… “Tunataka kujua kwa nini Serikali haikupeleka malalamiko yake MCT?”
Maandamano ya nchi nzima palepale
Sungura alisema pia kuwa vyama vyao vitatu vinaendelea na maandalizi ya maandamano ya nchi nzima yatakayofanyika Oktoba 10, mwaka huu.
Maandamano hayo yana lengo la kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete asisaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013.
Sungura alisema kuwa maandamano hayo yataandaliwa kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa.

SOURCE: MWANANCHI