Thursday 24 October 2013

Nimebambikiziwa kesi ya mauaji, adai Makongoro


Na Tausi Ally, Mwananchi

Posted  Alhamisi,Oktoba24  2013  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Kabla ya madai hayo, Hakimu Mkazi, Hellen Liwa aliuuliza upande wa mashtaka kuhusu ulipofikia upelelezi wa kesi hiyo.

Dar es Salaam. Mshtakiwa Makongoro Joseph Nyerere, anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya kukusudia katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, amelalamika kuwa amebambikiziwa kesi hiyo.
Alidai kitendo hicho kilikuja baada ya kukataa kutoa rushwa ya Sh 8 milioni polisi.
Madai hayo aliyatoa jana mbele ya Hakimu Mkazi, Hellen Liwa, wakati kesi hiyo ilipofikishwa kwa kutajwa.
Makongoro na mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, Abubakar Marijan (50), maarufu Papaa Msofe wanashtakiwa kwa tuhuma za kumuua mfanyabiashara wa madini, Onesphory Kituli mwaka 2011.
Kabla ya madai hayo, Hakimu Mkazi, Hellen Liwa aliuuliza upande wa mashtaka kuhusu ulipofikia upelelezi wa kesi hiyo.
Upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado unaendelea na baada ya maelezo hayo, mshtakiwa Makongoro alianza kulalamika.
“Mheshimiwa mimi kesi hii nimebambikiwa baada ya kukataa kutoa rushwa ya Sh8 milioni, naomba mahakama itumie mamlaka yake kuona haki inatendeka,” alilalamika Makongoro.
Alidai kuwa upande wa mashtaka umekuwa ukitoa taarifa zinazokinzana kuhusu upelelezi.

SOURCE: MWANANCHI