Thursday 7 November 2013

Rais Kikwete: Tanzania haiko tayari kujitoa kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki


Rais Jakaya Kikwete 



Posted  Alhamisi,Novemba7  2013  saa 18:1 PM
Kwa ufupi
Rais Jakaya Kikwete amelihutubia Bunge mjini Dodoma na kueleza kuwa Serikali ya Tanzania haiko tayari kujitoa katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Rais Jakaya Kikwete amelihutubia Bunge mjini Dodoma na kueleza kuwa Serikali ya Tanzania haiko tayari kujitoa katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
Rais Kikwete alibainisha kwamba kumekuwa na vikao visivyo rasmi vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wakuu wa Kenya, Uganda na Rwanda ambavyo vimekuwa vikipitisha mambo yao bila kushirikisha nchi nyingine ndani ya Jumuiya ambazo ni Tanzania na Burundi.
“Wenzetu wameshafanya vikao vitatu na kupitisha maamuzi manane ya kushirikiana, kwetu sisi tunadhani hizi ni fujo za kutaka kuhatarisha uhai wa maisha ya jumuiya yetu ya Afrika Mashariki," alisema Rais Kikwete.
Alisema Tanzania itaendelea kuheshimu mambo yaliyomo kwenye makubaliano ya uanzishwaji wa jumuiya hiyo ambayo ni umoja wa forodha, soko la pamoja, sarafu ya pamoja na shirikisho la kisiasa bila kukiuka mlolongo wa utekelezaji wake.
Mbali na suala la Jumuiya ya Afrika Mashariki, pia Rais Kikwete alizungumzia suala la wanajeshi waliokwenda nchini Congo DRC kulinda amani, Operesheni Tokomeza dhidi ya ujangili na mchakato wa Katiba Mpya
Kwa habari zaidi ungana nasi baadaye 

SOURCE: MWANANCHI