Monday 21 October 2013

Sofia Simba, Mwanjelwa ‘wamnanga’ Sugu


Na Godfrey Kahango, Mwananchi

Posted  Jumatatu,Oktoba21  2013  saa 10:17 AM
Kwa ufupi
Viongozi hao walisema kuwa wananchi wa jiji hilo wamepeleka ‘pepo’ bungeni ndio maana mbunge  huyo amekuwa kinara wa vurugu ndani ya Bunge, hivyo wananchi wa Mbeya Mjini wamempeleka mtu anayehitaji kuombewa.


Mbeya. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT), Sofia Simba na Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa waMbeya, Dk Mary Mwanjelwa (CCM), juzi walitumia muda mwingi jukwaani kumnangaMbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Chadema) wakimfananisha na `pepo’ aliyekwenda bungeni kwa ajili ya kufanya vurugu.
Viongozi hao walisema kuwa wananchi wa jiji hilo wamepeleka ‘pepo’ bungeni ndio maana mbunge  huyo amekuwa kinara wa vurugu ndani ya Bunge, hivyo wananchi wa Mbeya Mjini wamempeleka mtu anayehitaji kuombewa.
Walitoa kauli hiyo juzi wakati wakihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la wazi la Kata ya Manga
Mjini Mbeya.
Simba, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, alisema hali hiyo ya ‘mapepo’ mara kadhaa imekuwa  ikimsababishia mbunge huyo kujiingiza kwenye vitendo vya vurugu, likiwemo tukio la hivi karibuni kupigana bungeni badala ya kuibua hoja za maendeleo. Juhudi za gazeti hili za kumtafuta Sugu zilikwama jana baada ya kuelezwa na watu wake wa karibu kuwa alikuwa safarini China.
Simba alisema tukio la mbunge huyo kupigana na askari wa bunge ndani ya ukumbi, lilitokea kwa kuwa hakukuwa na mtu wa kuombea ‘mapepo’ siku hiyo baada ya kumkumba ghafla mbunge huyo.
 “Siku ile tukio linatokea bahati mbaya sana  Mchungaji  Lwakakatare (Mbunge  wa Viti Maalumu Getrud Lwakatare) hakuwemo ukumbini maana angeweza kuyaombea na hivyo naomba wananchi wa Mbeya msituletee ‘mapepo,” alisema.

SOURCE: MWANANCHI