31 Agosti, 2013 - Saa 13:30 GMT
                  

Wasomi, wasanii na 
wafanya-biashara wa Somalia wamekuwa wakizungumza katika mji mkuu, 
Mogadishu, kwenye ile mikutano inayofanywa sehemu mbali-mbali za dunia 
iitwayo TED-EX.
Mazungumzo hayo yaliyofanywa kwenye ukumbi wa 
mikutano chini ya ulinzi mkubwa, yalihusu mapendekezo na ubunifu wa 
kuijenga tena Somalia.Hotuba katika vikao vya TED-EX zimetolewa katika nchi zaidi ya 150.
source: BBC Swahili
