Kwa ufupi
Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni kati ya viongozi 
ambao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa kauli juu ya hali elimu 
nchini hususan kwenye nyanja ya sayansi na teknolojia.
Mwaka 2008 akiwa Bungeni Mjini  Dodoma, alieleza 
kwa undani kuhusu masomo ya Sayansi na Hisabati akitoa tahadhari ya 
kukosa wanasayansi ambao ni watu muhimu katika maendeleo.
Katika maelezo yake, analinganisha ufaulu  wa 
masomo ya sayansi na sanaa katika shule za msingi na sekondari, ambako 
ilithibitika kwamba ufaulu wa masomo ya sayansi kwa kipindi cha kuanzia 
mwaka 2003 hadi 2007 ulikuwa umeshuka.
Akifafanua zaidi  anasema, mwaka 2001, katika 
mtihani wa kumaliza darasa la saba, asilimia 62 ya watahiniwa katika 
Wilaya ya Morogoro Vijijini walipata sifuri katika mtihani wa Hisabati.
Anaeleza kuwa katika mtihani wa kidato cha nne 
mwaka 2007, matokeo yanaonyesha kwamba asilimia 69 ya watahiniwa 
walishindwa mtihani wa Hisabati.
“Katika zama hizi za sayansi na teknolojia, hali kama hii inatisha na haiwezi kuruhusiwa kuendelea kutokea,” anasema Pinda.
Kutokana na hali hiyo, Serikali imekuwa ikifanya 
jitihada mbalimbali za kufungua milango kwa wadau ambao wanaweza 
kuchochea maendeleo ya sayansi nchini.
Moja ya njia hizo ni mkutano wa wadau wa sayanasi 
 ‘Smart Partnership Dialogue’ uliohusisha wadau kutoka kwenye mataifa 
mbalimbali ya Afrika, lengo likiwa ni kujadili jinsi bara hili 
litakavyoweza kutumia teknolijia kuchangia maenedeleo.
Mbali na mkutano huo ambao, wadau mbalimbali 
walishauri Serikali kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja
 na kutenga fedha za kutosha ili kuwezesha tafiti kufanyika katika vyuo 
na taasisi nyingine.
Mbali na mkutano huo, taasisi isiyo ya kiserikali 
inayojishughulisha na tafiti zenye mweelekeo wa kisera kwenye masuala ya
 Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STIPRO), inawakutanisha wadau  wa sekta
 ya elimu kujifunza jinsi ya utoaji wa elimu ya uvumbuzi katika elimu ya
 juu na vyuo vya ufundi nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa STIPRO, Dk Britrina 
Diyamett anasema, mazingira yaliyopo katika elimu ya juu na vyuo vya 
ufundi hayakidhi matakwa ya utoaji wa elimu ya uvumbuzi.
“Vyuo vyetu bado havina vifaa vya kujifunzia na 
kufundishia, walimu nao hawajaandaliwa kutoa elimu ya uvumbuzi, 
wanafundishwa kinadhalia kuliko vitendo. Tutafute vifaa vya kujifunzia 
ili mwanafunzi anapomaliza kufundishwa kwa nadhalia, ajifunze pia kwa 
vitendo.” Anasema Dk Diyamett
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Aalbolrg Nchini Denmark, Profesa 
Palle Rasmussen anasema wanafunzi wanatakiwa kutambua umuhimu wa 
uvumbuzi na lengo la kukuza teknolojia.
Profesa Rasmussen anafafanua kuwa kunahitajika 
kutumia vitendo zaidi katika kufundisha na kuwashirikisha wadau wa sekta
 binafsi ili kuweza kufikia lengo la kuwa na wataalamu wa kutosha.
“Ili kuweza kutengeneza mfumo mzuri wa kuwapata wahitimu bora
 ni lazima kuwashirikisha wanafunzi na walimu wao katika utoaji na 
upokeaji wa mafunzo hayo ya uvumbuzi,” anasema Profesa Rasmussen.
Profesa Rasmussen anasema kuwa, taasisi za elimu zinaweza kuendesha tasinia ya uvumbuzi pasipo kutegemea serikali.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), 
Dk Johnson Ishengoma anasema, haiwezekani kujenga vijana kuwa wavumbuzi 
wakati miundombinu ya kujifunzia bado haijaimarishwa.
Anaeleza kuwa Serikali inatakiwa kuwekeza fedha za
 kutosha katika vyuo  ili kuviwezesha kufanya tafiti zitakazosadia 
kuvumbua mambo mbalimbali yenye tija kwa taifa.
 “Itachukua muda mrefu kutoa elimu bora ya 
uvumbuzi kutokana na kutokuwapo kwa walimu wa kutosha wa kutoa mafunzo 
hayo,” anasema Dk Ishengoma.
Dk Isengamo anaeleza kuwa elimu hiyo ikitolewa 
ipaswavyo, mwanafunzi akihitimu mafunzo yake ya chuo hatasubiri 
kuajiriwa na badala yake atajiajiri mwenyewe.
Naye Vera Mugittu kutoka Muvek Development 
Solutions Ltd anasema, anasema ni vigumu kutengeneza mfumo huo kutokana 
na kutokuwepo kwa sera inayoratibu utoaji wa mafunzo hayo.
“Utoaji wa elimu ya uvumbuzi ni jambo gumu na la 
muda mrefu, serikali inatakiwa kutambua umuhimu wake na kuwekeza zaidi 
kwa kutenga fedha za kutosha,” anasema Vera.
Mhadhiri wa Kuchuo Kikuu Cha Dar es Salaam, 
kitengo cha  cha uhandisi na ueknolojia, Profesa Bavo Nyichomba anasema 
kukuwa kwa uvumbuzi kunategemea na ongezeko la wanafunzi wanaosoma 
masomo ya sayansi.
Anasema ubora wa uvumbuzi umekuwa hauna tija kutokana na viwanda vilivyokuwapo hapo awali kufungwa.
“Ni jambo la aibu hadi vijiti vya meno na viwembe tunategemea kutoka nje, vitu ambavyo kama viwanda vyetu vingeimarishwa na kujengewa uwezo tumepiga hatua katika uvumbuzi,” anasema Profesa Nyichomba na kuongeza:
“Ni jambo la aibu hadi vijiti vya meno na viwembe tunategemea kutoka nje, vitu ambavyo kama viwanda vyetu vingeimarishwa na kujengewa uwezo tumepiga hatua katika uvumbuzi,” anasema Profesa Nyichomba na kuongeza:
“Tuanze kuboresha uvumbuzi kwa kuwarejesha 
wataalamu waliopo nje, waajiriwe na kutoa mafunzo sambamba na kutenga 
fedha za kutosha kuwezesha elimu ya juu na vyuo vya ufundi kutoa mafunzo
 kwa kiwango cha juu.”
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru 
Kawambwa anasema, jukumu la kutoa  elimu siyo la serikali pekee bali 
kila mwananchi ana mchango kwenye suala hilo.
 “Ili kutoa elimu iliyo bora ni jukumu la kila 
mmoja wetu, suala hili linahusisha nyanja mbalimbali. Kila mtu ana 
mchango katika kuhakikisha elimu yetu inakuwa bora. Walimu, wanafunzi 
na  wazazi kila mmoja akitekeleza wajibu wake ipasavyo tutafikia 
malengo,” anasema Dk Kawambwa.
chanzo: Mwananchi news paper
chanzo: Mwananchi news paper
 
  