Wanajeshi wa JWTZ wakibeba jeneza lenye mmoja wa askari wenzao saba 
waliouawa kwa shambulio la ghafla wakiwa katika Jeshi la Ulinzi wa Amani
 la Umoja wa Mataifa mjini Darfur, jumamosi iliyopita. Miili hiyo 
iliwasili leo Jumamosi, tarehe 20, saa 10.30 jioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Kikosi cha Anga 
cha JWTZ.
Baadhi ya viongozi wakiongozwa na Makamu wa Rais Dk. Muhammed Gharib 
Bilal wakishuhudia miili ya wanajeshi saba wa JWTZ waliouawa na waasi 
mjini Darfur, miili hiyo ilipofikishwa leo Uwanja wa Ndeje wa Kikosi cha
 anga cha JWTZ jijini Dar es Salaam.
Askari wakiingiza mwili mmoja wapo kati ya miili saba katika gari la jeshi tayari kuisafirisha.
Baadhi ya wananchi wakiwa hawaamini wanchokiona
 Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi 
Job Masima wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kikosi cha Anga cha JWTZ, kabla ya 
miili kuwasili. Wengine kulia ni Ridhiwani Jakaya Kikwete, Katibu wa 
NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa CCM 
(Bara), Mwigulu Nchemba. ambao walihudhuria mapokezi ya miili hiyo.
Makamu wa Rais, Dk. Muhammed Gharib Bilal akimsalimia Katibu Mkuu wa 
CCM, Kanali Mstaafu, Abdurhaman Kinana, baada ya kuwasili kwenye 
mapokezi ya miili ya wanajeshi hao. Katikati ni Waziri wa Ulinzi Shamshi
 Vuai Nahodha
 Makamu wa Rais Dk. Muhammed Gharib Bilal akimsalimia Katibu wa NEC, 
Itikadi na Uenezi Nape Nnauyebaada ya kuwasili kwenye Mapokezi ya miili 
ya askari wa JWTZ waliouawa mjini Darfur
Makamu wa Rais, Dk. Muhamed Gharib Bilal akiagana na Mkuu wa Majeshi, 
Jenerali Davis Mwamunyange, baada ya mapokezi ya wanajeshi wa JWTZ 
waliouawa Darfur kukamilika
 Ndugu wa mmoja wa askari wa JWTZ waliopoteza maisha kwa kushambuliwa na
 waasi mjini Darfur akiwa mwenye majozi wakati wa mapokezi ya askari 
hao.
Msafara wa malori saba yaliyobeba miili ya askari saba wa JWTZ waliouwa 
Darfur uliongozwa na polisi wakati wa kutoka Uwanja wa Ndege, Kikosi cha
 Anga baada ya kupokewa leo jioni. 
Picha zote na theNkoromo Blog










