“Unaposema huna imani na JWTZ, Polisi wetu unataka kuanzisha vikundi vya
 kukulinda tafsiri yake ni kwamba unataka kuanzisha vikundi vyenye sare 
hii si sahihi,”
Peter Kisumo 
            
Kwa ufupi
Akizungumza na gazeti hili jana, Kisumo alisema
 kauli ya Mbowe inamaanisha anataka kupata msaada wa vijana wake 
kufundishwa kumlinda yeye na kuhoji ni nchi gani inafadhili chokochoko 
hizo.
Moshi. Mwanasiasa mkongwe 
nchini, Peter Kisumo, amemvaa Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman 
Mbowe akimtaka aache kile alichodai ni kuitumbukiza nchi kwenye 
machafuko.
 “Unaposema huna imani na JWTZ, huna imani na 
Polisi wetu unataka kuanzisha vikundi vya kukulinda tafsiri yake ni 
kwamba unataka kuanzisha vikundi vyenye sare hii si sahihi,” alisema.
Akizungumza na gazeti hili jana, Kisumo alisema 
kauli ya Mbowe inamaanisha anataka kupata msaada wa vijana wake 
kufundishwa kumlinda yeye na kuhoji ni nchi gani inafadhili chokochoko 
hizo.
“Zipo nchi zina mapesa mengi na zipo tayari 
kufadhili machafuko nchi nyingine lakini nchi zilizostaarabika kama 
Ujerumani, Marekani, Uingereza na nyingine haziwezi kujiingiza huko,” 
alisema.
Alisema anaamini hata
 Ujerumani ambayo imekuwa ikikifadhili Chadema, haitakubali kutoa fedha 
kufadhili uanzishwaji wa vikundi hivyo vya ulinzi wakati vyombo halali 
vya ulinzi ni Polisi na JWTZ.
Kisumo alifafanua kuwa vyama vya siasa vina sare 
zake na kusema CCM, Chadema na Cuf navyo vina sare lakini kutaka 
kuanzisha vikundi vya ulinzi inamaanisha vitapaswa kuwa na sare za 
kijeshi.
  Kwa mujibu wa Kisumo, anaamini vyombo vya ulinzi
 na usalama nchini havitaruhusu kutekelezwa kwa mpango huo kwani 
unalenga kuwachochea wafuasi wa Chadema kutokutii mamlaka ya dola.
Suala la Chadema kutangaza mpango wake wa 
kuanzisha vikundi vya ulinzi limeibua mjadala mkali kati yake na CCM 
ambacho kinamiliki kikundi cha Green Guard huku Chadema wakimiliki Red 
Brigad
 
  